Winamp Logo
Ni Salama Cover

Ni Salama

Swahili, Religion, 1 season, 50 episodes, 8 hours, 35 minutes
About
Ni salama rohoni mwangu ni Podcast inayokusaidia kuboresha mahusiano yako na Mungu kupitia mafundisho mbalimbali yanayotolewa na wahubiri, walimu na wachungaji kiganjani mwako. Tunakusaidia kuweza kuanza siku vyema ukiwa na neno la mungu kama taa itakayokuwa ikikuongoza katika shughuli zako za kila siku. Kupitia Ni Salama tutakuletea mafunzo na masomo yatakayokuwezesha kuelewa zaidi neno la Mungu linalopatikana kwenye Biblia huku tukikuongezea hamu na mvuto wa kuisoma Biblia yako. Karibu
Episode Artwork

Semina ya wanaume Kawe 2019: 29

Kulingana na utakavyoguswa Moyoni mwako na ukataka kujiunganisha na Huduma ya Mana, unaweza kutuma sadaka kwa njia zifuatazo:Bwana Yesu Asifiwe!!Hizi ndizo namba za simu za huduma: +255754211633,+255715511633 na +255682657080.Tafadhali tunaomba usipige ila unaweza kutuma ujumbe mfupi (SMS) kama una hitaji lolote na litaombewa. Pia unaweza kutuma sadaka yako kupitia M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money.
11/30/202319 minutes, 27 seconds
Episode Artwork

Semina ya wanaume Kawe 2019: 28

Kulingana na utakavyoguswa Moyoni mwako na ukataka kujiunganisha na Huduma ya Mana, unaweza kutuma sadaka kwa njia zifuatazo:Bwana Yesu Asifiwe!!Hizi ndizo namba za simu za huduma: +255754211633,+255715511633 na +255682657080.Tafadhali tunaomba usipige ila unaweza kutuma ujumbe mfupi (SMS) kama una hitaji lolote na litaombewa. Pia unaweza kutuma sadaka yako kupitia M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money.
7/26/202110 minutes, 4 seconds
Episode Artwork

Semina ya wanaume Kawe 2019: 27

Kulingana na utakavyoguswa Moyoni mwako na ukataka kujiunganisha na Huduma ya Mana, unaweza kutuma sadaka kwa njia zifuatazo:Bwana Yesu Asifiwe!!Hizi ndizo namba za simu za huduma: +255754211633,+255715511633 na +255682657080.Tafadhali tunaomba usipige ila unaweza kutuma ujumbe mfupi (SMS) kama una hitaji lolote na litaombewa. Pia unaweza kutuma sadaka yako kupitia M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money.
7/26/202110 minutes, 3 seconds
Episode Artwork

Semina ya wanaume Kawe 2019: 26

Kulingana na utakavyoguswa Moyoni mwako na ukataka kujiunganisha na Huduma ya Mana, unaweza kutuma sadaka kwa njia zifuatazo:Bwana Yesu Asifiwe!!Hizi ndizo namba za simu za huduma: +255754211633,+255715511633 na +255682657080.Tafadhali tunaomba usipige ila unaweza kutuma ujumbe mfupi (SMS) kama una hitaji lolote na litaombewa. Pia unaweza kutuma sadaka yako kupitia M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money.
7/26/202110 minutes
Episode Artwork

Semina ya wanaume Kawe 2019: 25

Kulingana na utakavyoguswa Moyoni mwako na ukataka kujiunganisha na Huduma ya Mana, unaweza kutuma sadaka kwa njia zifuatazo:Bwana Yesu Asifiwe!!Hizi ndizo namba za simu za huduma: +255754211633,+255715511633 na +255682657080.Tafadhali tunaomba usipige ila unaweza kutuma ujumbe mfupi (SMS) kama una hitaji lolote na litaombewa. Pia unaweza kutuma sadaka yako kupitia M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money.
7/26/202110 minutes
Episode Artwork

Semina ya wanaume Kawe 2019: 24

Kulingana na utakavyoguswa Moyoni mwako na ukataka kujiunganisha na Huduma ya Mana, unaweza kutuma sadaka kwa njia zifuatazo:Bwana Yesu Asifiwe!!Hizi ndizo namba za simu za huduma: +255754211633,+255715511633 na +255682657080.Tafadhali tunaomba usipige ila unaweza kutuma ujumbe mfupi (SMS) kama una hitaji lolote na litaombewa. Pia unaweza kutuma sadaka yako kupitia M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money.
7/26/20219 minutes, 49 seconds
Episode Artwork

Semina ya wanaume Kawe 2019: 23

Kulingana na utakavyoguswa Moyoni mwako na ukataka kujiunganisha na Huduma ya Mana, unaweza kutuma sadaka kwa njia zifuatazo:Bwana Yesu Asifiwe!!Hizi ndizo namba za simu za huduma: +255754211633,+255715511633 na +255682657080.Tafadhali tunaomba usipige ila unaweza kutuma ujumbe mfupi (SMS) kama una hitaji lolote na litaombewa. Pia unaweza kutuma sadaka yako kupitia M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money.
7/26/202110 minutes, 12 seconds
Episode Artwork

Semina ya wanaume Kawe 2019: 22

Kulingana na utakavyoguswa Moyoni mwako na ukataka kujiunganisha na Huduma ya Mana, unaweza kutuma sadaka kwa njia zifuatazo:Bwana Yesu Asifiwe!!Hizi ndizo namba za simu za huduma: +255754211633,+255715511633 na +255682657080.Tafadhali tunaomba usipige ila unaweza kutuma ujumbe mfupi (SMS) kama una hitaji lolote na litaombewa. Pia unaweza kutuma sadaka yako kupitia M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money.
7/18/20218 minutes, 38 seconds
Episode Artwork

Semina ya wanaume Kawe 2019: 21

Kulingana na utakavyoguswa Moyoni mwako na ukataka kujiunganisha na Huduma ya Mana, unaweza kutuma sadaka kwa njia zifuatazo:Bwana Yesu Asifiwe!!Hizi ndizo namba za simu za huduma: +255754211633,+255715511633 na +255682657080.Tafadhali tunaomba usipige ila unaweza kutuma ujumbe mfupi (SMS) kama una hitaji lolote na litaombewa. Pia unaweza kutuma sadaka yako kupitia M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money.
7/18/202110 minutes, 51 seconds
Episode Artwork

Semina ya wanaume Kawe 2019: 20

Kulingana na utakavyoguswa Moyoni mwako na ukataka kujiunganisha na Huduma ya Mana, unaweza kutuma sadaka kwa njia zifuatazo:Bwana Yesu Asifiwe!!Hizi ndizo namba za simu za huduma: +255754211633,+255715511633 na +255682657080.Tafadhali tunaomba usipige ila unaweza kutuma ujumbe mfupi (SMS) kama una hitaji lolote na litaombewa. Pia unaweza kutuma sadaka yako kupitia M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money.
7/18/20219 minutes, 59 seconds
Episode Artwork

Semina ya wanaume Kawe 2019: 19

Kulingana na utakavyoguswa Moyoni mwako na ukataka kujiunganisha na Huduma ya Mana, unaweza kutuma sadaka kwa njia zifuatazo:Bwana Yesu Asifiwe!!Hizi ndizo namba za simu za huduma: +255754211633,+255715511633 na +255682657080.Tafadhali tunaomba usipige ila unaweza kutuma ujumbe mfupi (SMS) kama una hitaji lolote na litaombewa. Pia unaweza kutuma sadaka yako kupitia M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money.
7/18/202110 minutes, 8 seconds
Episode Artwork

Semina ya wanaume Kawe 2019: 18

Kulingana na utakavyoguswa Moyoni mwako na ukataka kujiunganisha na Huduma ya Mana, unaweza kutuma sadaka kwa njia zifuatazo:Bwana Yesu Asifiwe!!Hizi ndizo namba za simu za huduma: +255754211633,+255715511633 na +255682657080.Tafadhali tunaomba usipige ila unaweza kutuma ujumbe mfupi (SMS) kama una hitaji lolote na litaombewa. Pia unaweza kutuma sadaka yako kupitia M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money.
7/18/202110 minutes
Episode Artwork

Semina ya wanaume Kawe 2019: 17

Kulingana na utakavyoguswa Moyoni mwako na ukataka kujiunganisha na Huduma ya Mana, unaweza kutuma sadaka kwa njia zifuatazo:Bwana Yesu Asifiwe!!Hizi ndizo namba za simu za huduma: +255754211633,+255715511633 na +255682657080.Tafadhali tunaomba usipige ila unaweza kutuma ujumbe mfupi (SMS) kama una hitaji lolote na litaombewa. Pia unaweza kutuma sadaka yako kupitia M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money.
7/18/202110 minutes, 1 second
Episode Artwork

Semina ya wanaume Kawe 2019: 16

Kulingana na utakavyoguswa Moyoni mwako na ukataka kujiunganisha na Huduma ya Mana, unaweza kutuma sadaka kwa njia zifuatazo:Bwana Yesu Asifiwe!!Hizi ndizo namba za simu za huduma: +255754211633,+255715511633 na +255682657080.Tafadhali tunaomba usipige ila unaweza kutuma ujumbe mfupi (SMS) kama una hitaji lolote na litaombewa. Pia unaweza kutuma sadaka yako kupitia M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money.
7/18/20219 minutes, 58 seconds
Episode Artwork

Semina ya wanaume Kawe 2019: 15

Kulingana na utakavyoguswa Moyoni mwako na ukataka kujiunganisha na Huduma ya Mana, unaweza kutuma sadaka kwa njia zifuatazo:Bwana Yesu Asifiwe!!Hizi ndizo namba za simu za huduma: +255754211633,+255715511633 na +255682657080.Tafadhali tunaomba usipige ila unaweza kutuma ujumbe mfupi (SMS) kama una hitaji lolote na litaombewa. Pia unaweza kutuma sadaka yako kupitia M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money.
7/18/202110 minutes, 2 seconds
Episode Artwork

Semina ya wanaume Kawe 2019: 14

Kulingana na utakavyoguswa Moyoni mwako na ukataka kujiunganisha na Huduma ya Mana, unaweza kutuma sadaka kwa njia zifuatazo:Bwana Yesu Asifiwe!!Hizi ndizo namba za simu za huduma: +255754211633,+255715511633 na +255682657080.Tafadhali tunaomba usipige ila unaweza kutuma ujumbe mfupi (SMS) kama una hitaji lolote na litaombewa. Pia unaweza kutuma sadaka yako kupitia M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money. 
7/15/202117 minutes, 35 seconds
Episode Artwork

Semina ya wanaume Kawe 2019: 13

Kulingana na utakavyoguswa Moyoni mwako na ukataka kujiunganisha na Huduma ya Mana, unaweza kutuma sadaka kwa njia zifuatazo:Bwana Yesu Asifiwe!!Hizi ndizo namba za simu za huduma: +255754211633,+255715511633 na +255682657080.Tafadhali tunaomba usipige ila unaweza kutuma ujumbe mfupi (SMS) kama una hitaji lolote na litaombewa. Pia unaweza kutuma sadaka yako kupitia M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money.
7/14/20218 minutes, 9 seconds
Episode Artwork

Semina ya wanaume Kawe 2019: 12

Kulingana na utakavyoguswa Moyoni mwako na ukataka kujiunganisha na Huduma ya Mana, unaweza kutuma sadaka kwa njia zifuatazo:Bwana Yesu Asifiwe!!Hizi ndizo namba za simu za huduma: +255754211633,+255715511633 na +255682657080.Tafadhali tunaomba usipige ila unaweza kutuma ujumbe mfupi (SMS) kama una hitaji lolote na litaombewa. Pia unaweza kutuma sadaka yako kupitia M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money.
7/14/20219 minutes, 46 seconds
Episode Artwork

Semina ya wanaume Kawe 2019: 11

Kulingana na utakavyoguswa Moyoni mwako na ukataka kujiunganisha na Huduma ya Mana, unaweza kutuma sadaka kwa njia zifuatazo:Bwana Yesu Asifiwe!!Hizi ndizo namba za simu za huduma: +255754211633,+255715511633 na +255682657080.Tafadhali tunaomba usipige ila unaweza kutuma ujumbe mfupi (SMS) kama una hitaji lolote na litaombewa. Pia unaweza kutuma sadaka yako kupitia M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money.
7/14/202111 minutes, 42 seconds
Episode Artwork

Semina ya wanaume Kawe 2019: 10

Kulingana na utakavyoguswa Moyoni mwako na ukataka kujiunganisha na Huduma ya Mana, unaweza kutuma sadaka kwa njia zifuatazo:Bwana Yesu Asifiwe!!Hizi ndizo namba za simu za huduma: +255754211633,+255715511633 na +255682657080.Tafadhali tunaomba usipige ila unaweza kutuma ujumbe mfupi (SMS) kama una hitaji lolote na litaombewa. Pia unaweza kutuma sadaka yako kupitia M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money.
7/14/20219 minutes, 14 seconds
Episode Artwork

Semina ya wanaume Kawe 2019: 9

Kulingana na utakavyoguswa Moyoni mwako na ukataka kujiunganisha na Huduma ya Mana, unaweza kutuma sadaka kwa njia zifuatazo:Bwana Yesu Asifiwe!!Hizi ndizo namba za simu za huduma: +255754211633,+255715511633 na +255682657080.Tafadhali tunaomba usipige ila unaweza kutuma ujumbe mfupi (SMS) kama una hitaji lolote na litaombewa. Pia unaweza kutuma sadaka yako kupitia M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money.
7/14/202110 minutes, 12 seconds
Episode Artwork

Semina ya wanaume Kawe 2019: 8

Kulingana na utakavyoguswa Moyoni mwako na ukataka kujiunganisha na Huduma ya Mana, unaweza kutuma sadaka kwa njia zifuatazo:Bwana Yesu Asifiwe!!Hizi ndizo namba za simu za huduma: +255754211633,+255715511633 na +255682657080.Tafadhali tunaomba usipige ila unaweza kutuma ujumbe mfupi (SMS) kama una hitaji lolote na litaombewa. Pia unaweza kutuma sadaka yako kupitia M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money.
7/14/202112 minutes, 25 seconds
Episode Artwork

Semina ya wanaume Kawe 2019: 7

Kulingana na utakavyoguswa Moyoni mwako na ukataka kujiunganisha na Huduma ya Mana, unaweza kutuma sadaka kwa njia zifuatazo:Bwana Yesu Asifiwe!!Hizi ndizo namba za simu za huduma: +255754211633,+255715511633 na +255682657080.Tafadhali tunaomba usipige ila unaweza kutuma ujumbe mfupi (SMS) kama una hitaji lolote na litaombewa. Pia unaweza kutuma sadaka yako kupitia M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money.
7/9/20217 minutes, 42 seconds
Episode Artwork

Semina ya wanaume Kawe 2019: 6

Kulingana na utakavyoguswa Moyoni mwako na ukataka kujiunganisha na Huduma ya Mana, unaweza kutuma sadaka kwa njia zifuatazo:Bwana Yesu Asifiwe!!Hizi ndizo namba za simu za huduma: +255754211633,+255715511633 na +255682657080.Tafadhali tunaomba usipige ila unaweza kutuma ujumbe mfupi (SMS) kama una hitaji lolote na litaombewa. Pia unaweza kutuma sadaka yako kupitia M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money.
7/9/202110 minutes, 13 seconds
Episode Artwork

Semina ya wanaume Kawe 2019: 5

Kulingana na utakavyoguswa Moyoni mwako na ukataka kujiunganisha na Huduma ya Mana, unaweza kutuma sadaka kwa njia zifuatazo:Bwana Yesu Asifiwe!!Hizi ndizo namba za simu za huduma: +255754211633,+255715511633 na +255682657080.Tafadhali tunaomba usipige ila unaweza kutuma ujumbe mfupi (SMS) kama una hitaji lolote na litaombewa. Pia unaweza kutuma sadaka yako kupitia M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money.
7/9/20219 minutes, 55 seconds
Episode Artwork

Semina ya wanaume Kawe 2019: 4

Kulingana na utakavyoguswa Moyoni mwako na ukataka kujiunganisha na Huduma ya Mana, unaweza kutuma sadaka kwa njia zifuatazo:Bwana Yesu Asifiwe!!Hizi ndizo namba za simu za huduma: +255754211633,+255715511633 na +255682657080.Tafadhali tunaomba usipige ila unaweza kutuma ujumbe mfupi (SMS) kama una hitaji lolote na litaombewa. Pia unaweza kutuma sadaka yako kupitia M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money.
7/9/202110 minutes, 4 seconds
Episode Artwork

Semina ya wanaume Kawe 2019: 3

Kulingana na utakavyoguswa Moyoni mwako na ukataka kujiunganisha na Huduma ya Mana, unaweza kutuma sadaka kwa njia zifuatazo:Bwana Yesu Asifiwe!!Hizi ndizo namba za simu za huduma: +255754211633,+255715511633 na +255682657080.Tafadhali tunaomba usipige ila unaweza kutuma ujumbe mfupi (SMS) kama una hitaji lolote na litaombewa. Pia unaweza kutuma sadaka yako kupitia M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money.
7/9/202110 minutes
Episode Artwork

Semina ya wanaume Kawe 2019: 2

Kulingana na utakavyoguswa Moyoni mwako na ukataka kujiunganisha na Huduma ya Mana, unaweza kutuma sadaka kwa njia zifuatazo:Bwana Yesu Asifiwe!!Hizi ndizo namba za simu za huduma: +255754211633,+255715511633 na +255682657080.Tafadhali tunaomba usipige ila unaweza kutuma ujumbe mfupi (SMS) kama una hitaji lolote na litaombewa. Pia unaweza kutuma sadaka yako kupitia M-Pesa, Tigo Pesa na Airtel Money.
7/9/20219 minutes, 59 seconds
Episode Artwork

Semina ya wanaume Kawe 2019

Somo hili si mali ya Ni Salama bali ni mali ya Christopher nad Diana Mwakasege. Kupata somo hili na mengine tafadhali wasiliana nao kupitia njia zilizopo hapo chini. Hili somo na mengine yaliyowekwa kwenye podcast hii hayana nia ya kupata pesa bali kwa kujisogeza karibu na Mungu kwa njia ya mafundisho kama hili unalosikiliza. Kwa sadaka na shukurani tafadhali ziwasilishe kwa huduma ya Mana, namba ziko kwenye masomo yanayoendelea. JINSI YA KUPATA MASOMO HAYA NA MENGINE MENGI KWA NJIA YA VITABU, KANDA, CDs & DVDs. Unaweza kutoa oda na ukatumiwa mafundisho hayo popote ulipo, kwa kupiga simu kila Jumatatu hadi Ijumaa kuanzia saa 3 asubuhi hadi saa 11 jioni kwenye namba zifuatazo: *1. Kwa walioko Arusha na maeneo mengine yote Tanzania wasiliana na Lucy: +255 736 501 081, au fika ofisi za MANA Arusha iliyoko eneo hili  👉🏼goo.gl/VQSmeB* 2. Kwa walioko Dar es Salaam na maeneo mengine yote Tanzania wasiliana na Dinna: +255 739 501 081 au fika ofisi za MANA Dar zilizo karibu na Posta ya Zamani, Jengo la Luther House, Ghorofa ya Tatu. Pia unaweza kutuandikia kwa EMAIL/BARUA PEPE: [email protected] Kwa maeneo mengine, unaweza kupata mafundisho mbali mbali moja kwa moja wakati wa kongamano au semina itakapofanyika kwenye mkoa/maeneo husika kwa kufika kwenye BANDA la VITABU, KANDA, CDs & DVDs pale UWANJANI na pia kutoa order na ukatengenezewa. (WAKATI WA SEMINA). https://goo.gl/JAGBSN  UBARIKIWE SANA     www.mwakasege.org
7/9/202110 minutes, 2 seconds
Episode Artwork

Namna ya kujiandaa kukikabili kipindi hiki cha siku za mwisho (Sehemu ya tatu)

Tutakusanyika mbele za Bwana tutaimba na kushangilia. Kama Yesu asingekufa msalabani safari yake ingekuwa bure. Maana angeishia kuponya watu na ingekuwa bure tu. Kama asingekufa na akafufuka ingekuwa shida sana. Biblia inasema ulitokea ubishi juu ya kiama ya wafu ule ubishi ulileta mtengano katika dini ya wayahudi na ukatengeneza dini ya masadukayo. Ugomvi wao ulikuwa ni imani yao juu ya kiama ya wafu. Huo ubishi ukaletea mgawanyo mpaka ndani ya kanisa wakati ambao watu wameanza kuokoka. Ilibidi Roho Mtakatifu amsemeshe Paulo aandike barua kwa Wakorintho ili wajue kuwa kama Kristo hakufufuka imani yetu ni bure maana yake haina faida. Kama Kristo hakufufuka tumekuwa masikini kuliko watu wote ambao tunamtegemea Bwana. Kama Kristo amefufuka tunajua na sisi kwamba atatufufua. Kwa sababu hiyo anasema ni tumaini lenye baraka kama ambavyo Tito alivyoandika. Endelea kuimba wimbo huo “Wateule wote tutakusanyika” Wimbo huu ukuandae kufanya sala ya toba. Kama uliokoka ukarudi nyuma rudi tena kwa Mungu. Pia kama unajua kabisa Yesu akija leo huna uhakika kama utaenda nae rudi kwa Bwana. Siku moja nilikuwa kwenye ndege mimi na Rubani mmoja. Tulikuwa wawili tu. Akaniambia akipata shida je ntafanyeje. Basi akaanza kunionesha namna ya kushika usukani wa ndege na namna ya kuendesha ndege. Akanionesha mpaka namna ya kutumia breki za ndege. Sasa nikatazama chini, niliona kulivyo mbali sana. Pia nikaona namna tunavyopita mawinguni. Ghafla nikakumbuka “mstari kuwa tutakusanyika kumlaki Bwana Mungu mawinguni”. Yule Rubani alikuwa kaokoka Nikamwambia kuwa ikipigwa tarumbeta ya kuondoka na Yesu akija hapa kutunyakua tutaenda naye na hii ndege itajijua itakakoenda. Lakini kama Mungu anataka tubaki tutabaki. Ni hatari sana kukaa dakika moja mahali na hujui kama Yesu akitokea hapa utaenda naye. Ni hatari sana kwa sababu Yesu yupo, hata kama huamini kama Yupo. Wainjilisti huwa wanatuambia kuwa kama utaamini Yesu yupo hutakuwa na hasara kama usipomkuta ila utakuwa na hasara sana kama utaamini hayupo halafu ukamkuta. Shida ya wengi wanataka waishi mpaka watakapokuwa wazee ile saa wanakaribia kufa ndipo wanatafuta mchungaji waokoke. Kijana wetu Joshua alikufa akiwa mdogo na wenzake wakaniuliza swali “Baba kwanini Mungu alimchukua Joshua akiwa bado mdogo sana wakati biblia inasema kuwa tunaweza kuishi miaka 70 na tukiwa na nguvu miaka 80. Sasa kwa nini Yeye amekufa mapema sana”. Nikawaambia ni kwa sababu mnasoma mstari mmoja tu. Biblia inasema nitakushibisha kwa wingi wa siku. Unaweza ukaishi miaka zaidi ya 80 au ukaishi chini ya hiyo miaka. Anayesema nimeshiba sio yule mgawaji wa chakula bali ni yule anayekula. Nikawaambia kitu kingine kuwa maisha ya mtu ni kitabu kila siku ni ukurasa. Ndio maana biblia inasema Mungu anatangaza mwisho tangu mwanzo. Kwa hiyo ukiona umezaliwa basi ujue kuwa Mungu alifika mwisho ndipo akaruhusu ukazaliwa na ukaanza kitabu chako cha maisha. Kuna maisha ambayo ni sura maana unaona kabisa hapa kuna ukurasa umeisha hapa ila unajua si ukurasa tu bali ni awamu ya maisha imeisha. Kila mwanadamu anayo hiyo. Mungu amendika siku zetu na ndiyo maana mtunga zaburi anasema Mungu naomba nisaidie kuzijua siku zangu. Kuna vitabu vingine vina kurasa chache sana na ni vitabu vitamu sana. Mwandishi hakuwa na sababu ya kuandika kitabu kikubwa wakati alichokuwa anatakiwa kuandika kimeisha. Kuna vitabu vingine vina kurasa nyingi sana na ukisoma ukurasa wa kwanza na wa pili unakifunga kwa sababu hakina ladha kwa sababu kama ukiandika tu kwa ajili ya kujaza kurasa hata wewe mwenyewe hutarudia kukisoma. Hivyo hivyo hata Mungu pia haandiki tu maisha ya mtu kwa ajili ya kujaza siku. Nikawaambia wale rafiki zake Joshua kuwa kitabu chake kilikuwa ni kifupi sana lakini ni kitamu. Maana kuna vitabu vingine vikiisha unatazama kama kuna mwendelezo wake maana ni kitamu sana. Hicho kitabu hukiachi mahali bali utakiweka mfukoni. Kila baada ya muda utakuwa unakisoma. Yesu hakumaliza miaka 40, na kitabu chake ni kitamu sana mpaka leo tunasoma na hatuchoki kusoma. Hakuna kitu kibaya kama nikikuuliza sasa hivi kuwa ukifa sasa utaenda wapi?. Kama huna jibu lililonyooka ujue unamhitaji Yesu. Maana hutaweza kwenda mbinguni kwa sababu ya mahali unaposali. Hakuna dini iliyokufa kwa ajili ya mtu. Na usije ukajivunia matendo mema maana wakovu ni kipawa hakiji kwa njia ya matendo mema bali ni kwa njia ya imani. Kama unajiona una matendo mema kasimame mbele za Mungu aliye Hai na ndipo utajua kama uko salama!. Kumbuka Isaya alihuburi sura ya kwa hadi sura ya tano. Sura ya sita baada ya kufa kwa mfalme Uzia ndipo alisema mimi ni “mwenye dhambi na midomo michafu”. Sura zote tano hakuona bali sura ya sita ndipo anaona ana mapungufu kwa sababu Mungu alijifunua kwake. Miaka kadhaa tukiwa Tanga kwenye semina nilikuwa nafundisha habari za Jina la Yesu. Ilikuwa ni semina ya siku tano tulikuwa ndani ya jengo. Jengo lile lilikuwa la wenzetu wa imani ya kihindi wanaobudu ng’ombe wakatupa jengo lao tukafanyia semina. Siku ya pili niliitwa Dar es Salaam kwenye masuala ya uchumi. Wazo la kwanza lilonijia ni kutokwenda Mungu akaniambia nenda kwa sababu ile kazi nayo pia nimekupa unatakiwa uende. Nikamuuliza sasa semina ya kesho? akasema upako wa kesho uko juu ya mke wako. Hata kama ningebaki upako ulikuwa juu ya mke wangu maana ndiye aliyekuwa anatakiwa kufundisha. Basi nilienda Dar es Salaam maana kikao kilikuwa saa nane hadi saa kumi, nilipomaliza nikarudi Tanga. Nilipofika ilikuwa majira ya saa tano usiku nikakuta mji umetahatuki, nguvu za Mungu zimeshuka pale watu wamejazwa Roho Mtakatifu sana. Kuna mtoto mmoja alinena kwa siku tatu. Watu walikuwa hawafiki nyumbani wanalala njiani wananena kwa lugha hata wanashindwa kuongea. Ile hali ilitutia hofu sana maana tuliona madhaifu tuliyo nayo na vitu ambavyo Mungu anafanya havifanani kabisa. Mungu alifanya vitu vikubwa sana. Tulienda kumuuliza Mungu na alitujibu mwezi wa kumi tukiwa Kilombero kuwa uchafu unaonekana mahali ambapo kuna nuru. Neno la Mungu na Roho Mtakatifu ni nuru. Mahali ambapo kuna uchafu baada ya kumulikwa na nuru ndipo utaanza kupafanyia usafi. Paulo kadri alivyokuwa anaenda mbele za Bwana aliona udhaifu aliokuwa nao.
8/15/201910 minutes, 5 seconds
Episode Artwork

Namna ya kujiandaa kukikabili kipindi hiki cha siku za mwisho (Sehemu ya pili)

Katika siku hizi za mwisho ambazo Yesu anakaribia kurudi dunia lazima ijue, mkubwa kwa mdogo lazima wajue kwamba kurudi kwa Bwana kumekaribia. Biblia inasema na watakatifu na wazidi kujitakasa, wanaofanya kazi ya Mungu na wafanye upesi maana Roho pamoja na malaika na watumishi wanasema njoo, maana yake kuna kitu kinachomzuia asije. Biblia inasema injili ya Ufalme wa Mungu itakapohubiwa kote, anasubiri tufanye kazi yake. Kama umesoma kitabu cha Luka wakati Yesu amefufuka Luka 24:44 Kisha akawaambia, Hayo ndiyo maneno yangu niliyowaambia nilipokuwa nikali pamoja nanyi, ya kwamba ni lazima yatimizwe yote niliyoandikiwa katika Torati ya Musa, na katika Manabii na Zaburi. Ndipo akawafunulia akili zao wapate kuelewa na maandiko. Akawaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu; na kwamba mataifa yote watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, kuanza tangu Yerusalemu. Nanyi ndinyi mashahidi wa mambo haya. Na tazama, nawaletea juu yenu ahadi ya Baba yangu; lakini kaeni humu mjini, hata mvikwe uwezo utokao juu. Akawaongoza mpaka Bethania, akainua mikono yake akawabariki. Ikawa katika kuwabariki, alijitenga nao; akachukuliwa juu mbinguni. Matendo ya mitume inasema malaika waliokuwepo pale wakawaambia wale watu kuwa kwa jinsi wanavyomwona anaenda ndivyo watakavyomwona anarudi. Kabla ya kuwaahidi Roho Mtakatifu aliwafunulia akili zao wapate kuelewa na maandiko. Kwa sababu unaweza ukawa na Roho Mtakatifu na usielewe maandiko kwa sababu Roho Mtakatifu anahitaji ushirika wa akili, kuonyesha kwamba Roho Mtakatifu anapoingia kazini lazima akili ziwe active. Kwa sababu huko ndiko kunakoelewa. Imani inaweza kukufanya kuchukua hatua ya kitu ambacho huelewi kwa sababu huwezi kuelewa kila kitu ambacho Mungu anakuambia fanya, vingine inahitaji kuchukua hatua kwa imani, lakini pia kudumu katika hicho alichokufanyia unahitaji kudumu katika Neno kwa sababu mtu hakuitwa kuishi kwa muujiza bali kwa Neno linalotoka katika pumzi ya Mungu. Ni rahisi kuwasisitizia watu miujiza ukasahau kusisitiza kwa Neno na kwa sababu hiyo wataweka imani kwenye miujiza na kusahau Neno na watu wataanza kutafuta miujiza ilipo kila mahali badala ya kutafuta Neno lilipo, na kwa sababu hiyo hawatajifunza kutegemea Neno watajifunza kutegemea watumishi. Roho inapopokea Neno inaligeuza kuwa imani na imani ni kuwa na uhakika wa mambo yatarajiwayo, unapewa Neno na kulifuata na kufanya, saa nyingine kuna vitu vingine hata huelewi inakuaje lakini unafuata tu kwa sababu Mungu ameweka hiyo makusudi kwa sababu kuna akili zingine hazijakaa sawa kuelewa. Nilienda nchi moja inaitwa Jamhuri ya Ireland ipo kaskazini magharibi mwa nchi ya Uingereza kwenye mji wake mkuu unaitwa Dublin. Nilikuwa na vikao vya kawaida na wafadhili mbali mbali wanaofadhili nchi mbali mbali zinazoendelea na Tanzania ikiwemo. Sikuenda kuiwakilisha serikali nilienda kwa sababu ya vitu ambavyo Mungu ameweka ndani yangu kufuatilia masuala ya uchumi. Kwa hiyo nikaenda kwenye hicho kikao nikawasikiliza wale wazungu kutoka mashirika na serikali mbali mbali wakieleza namna ya kuongeza misaada. Wakazungumza mipango mbali mbali juu ya nchi zinazoendelea wakati ule naenda Tanzania ulikuwa imeshapata Uhuru takribani mwaka wa 40. Wakati wao wanaongea mimi nalitazama kwa jinsi ya kibiblia, kwa hiyo nilishindwa kuvumilia nikanyosha mkono. Wakanipa nafasi ya kuongea nikawaambia ukiwa ni mzazi na una mtoto wa miaka 40 na umekuwa ukimsaidia kila wakati, na sisi kama Tanzania toka tupate uhuru mnatupa msaada tu ninyi hizi hela zenu zisizoisha mnazipata wapi?. Kwanini hamtufundishi mahali mnapata ili tusiwasumbue kila mara kuja kuomba misaada toka kwenu. Lakini hawawezi kutufundisha kwa sababu wataharibu uchumi wao. Mzungu moja ambaye tulikuwa tunashirikiana naye akaniminya kwenye suruali akaniambia Mwakasege usiseme namna hiyo, nikamwambia hapana lazima waseme hizi hela ambazo haziishi wanazipataje si watufundishe na sisi. Unaweza ukaomba kwa Mungu muujiza wa milioni moja kakupa, na unaweza kuomba kwa Mungu mbinu za kupata na mpango wa namna ya kupata milioni moja kila siku, je utataka kitu gani? (mbinu na mpango). Sasa kwa nini kukimbilia miujiza, Muujiza si mbaya maana muujiza uliwekwa kwa ajili ya Mungu kuingilia kati. Ni divine intervention, anaingilia kati kukusaidia lakini hakupanga uishi namna hiyo kwa kutegemea miujiza bali yeye ana mipango na mikakati kwa ajili yako. Ndio maana biblia haisemi kuwa najua miujiza niliyowapangia nyinyi asema Bwana, vinginevyo kila mtu angekuwa anaenda kwa Mungu kumkumbusha kuwa Mungu muujiza wangu uko wapi.
8/14/20199 minutes, 56 seconds
Episode Artwork

Namna ya kujiandaa kukikabili kipindi hiki cha siku za mwisho

Na Biblia inasema Yesu siku za mwisho hatakuja hapa duniani, kwa sababu maandiko yanasema kile kiti cha enzi kikubwa cheupe, kiti cha hukumu dunia itakimbia na mbingu zitakimbia na kwa sababu hiyo hicho kiti hakitakuwa duniani kwa sababu dunia itakimbia na mbingu zitakimbia. Biblia inasema nikawaona wafu wakubwa kwa wadogo wamesimama katika kiti cha enzi halafu atasimama pale kama hakimu. Sasa hivi ni mwokozi wako lakini ukikutana naye ng’ambo ya pili kama hujaokoka utakutana naye kama hakimu na maandiko yanasema atabagua na kuita majina. Biblia inasema mauti itaitwa iwatoe wafu, bahari na kuzimu itaitwa. Unajua saa nyingine tunafanya kazi ya Mungu tunasahau kuwaambia na kuwahimiza watu juu ya ukaribu wa kurudi kwa Yesu. Tangu watoto wetu wakiwa wadogo kati ya kitu ambacho tumekuwa tukiwasemesha mara kwa mara ni hiki. **Kwenye mambo ya rohoni waishi kama watakufa sasa hivi, na kwenye mambo ya mwilini waishi kama vile hawatakufa maana yake kwenye mambo ya rohoni waishi wakiwa tayari Yesu akishuka sasa hivi wawe tayari, hawana shida ya kutahayari wanaenda pamoja na Bwana, lakini waendelee kupanga maisha yao na kufanya shuguli zao na kupanga mambo mbalimbali kama vile kufa hakupo. ** Na watu wengi wanapanga mambo yao kama vile Yesu hatatokea wakati wowote ule. Na kitu mojawapo katika utumishi ukishapoteza sura ya kurudi kwa Yesu uwe na uhakika utapoteza na uchaji na utapoteza umuhimu wa nyakati, utataka kufanya vitu vyako saa yeyote unayotaka lakini huwezi kufanya kazi ya Mungu saa yeyote unayotaka, huwezi kutii kitu cha Mungu saa yeyote unayotaka. Mungu ameachia kila kitu kwa saa yake na mipango yake na anategemea watu wake sio tu watii Neno lake lakini watii Neno lake katika nyakati na muda aliowawekea kwa sababu nyakati na muda aliowawekea ndizo zinazoweka thamani ya Neno. Jaribu kuzungumza na mtu ambaye hajaokoka kabla hajafa halafu ukasema nina shughuli nyingi halafu kesho ukamkuta amekufa, thamani ya Neno lako la wokovu kwa yule mtu imepotea, lilikuwa na thamani jana alipokuwa hai. Thamani ya Neno liko kwenye muda, ndio anasema wape watu chakula kwa wakati. Shetani akitaka kuvuruga utumishi wako anakamata akili na kwenye akili anashika eneo linaloshughulika na nyakati kwa sababu akilishika hilo huna namna ya kupangua marafiki ambao sio wazuri. Biblia inasema huyu mtu ameshirikiana na watu ambao kwa jinsi ya kawaida asingeshirikiana nao kwa sababu ameona bwana wake amekawia. Maana yake ndani ya nafsi yake akili ziliposhikwa akapoteza kujua ya kwamba Yesu anaweza kutokea wakati wowote ule kwa hiyo akajikuta yuko na marafiki wa aina yeyote ile. Haiwezekani umsubiri Yesu mawinguni SAA yeyote, halafu ukae na mtu yeyote tu, kazi mojawapo ya akili ni kukuchagulia watu. Akili zikibanwa mtu yeyote tu ambaye anaweza kuwa karibu na wewe, anawaza kama wewe hutajua hata namna ya kujikung’uta naye, lakini ukijua ya kwamba Yesu anarudi, mwili unaweza ukapiga kelele unajua umechoka sana! Ni sawa umechoka lakini unaenda mbele za Bwana unakuta Roho Mtakatifu akikuhimiza siku za kurudi Bwana zimekaribia. Wengine wanamfahamu mzee moja aliitwa Aaron Mabondo wa kanisa la Pentecost kule Dar es salaam, ameshafariki sasa alitusaidia sana kwenye kukua ndani ya Bwana, siku alipokaribia kufariki tulienda kuongea naye, mwili wake ulikuwa umechoka, tulikuwa na mke wangu na mke wake alikuwa pale halafu akanitazama usoni akamtazama na mke wangu halafu akasema “wanangu mnisikie mnaniona jinsi nilivyo fanyeni kazi ya Bwana maadam mwili unawaruhusu kusonga mbele, songa mbele kwa sababu mtafika saa hamtaweza kutumika tena” hakumaliza mwezi akafa. Ukiwa na wazo la Yesu kurudi ukisikia basi limeanguka na kuua watu kumi wazo la kwanza ndani yako ni je wamekufa wanamjua Yesu?! Sio swala la huzuni ni swala la kwamba amekufaje! Ukiona ndani hilo swali halipo unahitaji kurudi kwa Bwana ujue akili zako zimebanwa. Kwa sababu shetani atakuchanganya kama sio kurudi kwa Yesu atakuchanganya kuchukua mafundisho ambayo sio sahihi. Atahakikisha anaondoa kitu cha kurudi kwa Yesu kisiwe sehemu ya maisha yako na wakati kinatakiwa kuwa sehemu ya maisha yako. Maana yake kaa mkao ili Yesu akikuitia mahali popote unaenda. Kitu mojawapo kilichomponza yule mtumishi akapelekwa mahali ambapo kuna kilio na kusaga meno ni kwamba alisema Bwana wake amachelewa kurudi. Akili zake zilimwingizia kitu cha tofauti, shetani alibadilisha mistari ile ambayo Mungu aliyompa Adamu maelekezo na alienda kwenye fikra, akaanza kuweka kiulizo kwenye ahadi ya Mungu na Neno la Mungu. Na huyu mtumishi Bwana wake amemwambia mimi karibu narudi niandalie watu wangu niandalie kanisa langu halafu yeye anasema bwana amekawia kurudi! Hilo wazo amelipata wapi? Lazima shetani ametumbukiza kitu kwenye fikra zake, anaanza kusema Yesu haji, mbona mwaka juzi, mwaka jana tumeendelea hivo hivo. Wewe unatazama vitu kwa jinsi ya mwili unasahau kwamba lazima utazame sehemu zote mbili kwa sababu kurudi kwa Bwana kunategemea, wengine siku atakapotokea atawakuta wakiwa hai na watabadilishwa miili yao kufumba na kufumbua watanyakuliwa, lakini kuna wengine wanatakiwa walale katika Bwana siyo katika dini, bali kuhakikisha kwamba una Yesu ndani yako. Ushuhuda Nilikuwa naongea na rafiki yangu moja niliyekuwa nafanya naye kazi ofisi moja mahali, halafu akaugua nikamfuata nyumbani kwake hajiwezi kabisa hata kusimama kwenye kitanda, nikamwambia “ndugu najua wewe ni Mkristo mzuri na tunasali wote lakini najua hujaokoka na mimi nataka nikuongoze sala ya toba umpokee Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yako. Huu ni mtaji, ni mtaji wa kuishi milele na pia ni mtaji wa kuishi na Yesu duniani, na akikuita saa hii ni mtaji wa kwenda mbinguni, je unasemaje?” akasema “Niko tayari”. Nikamwongoza sala ya toba kitandani na baada ya mwezi mmoja akafa.
8/13/201910 minutes, 13 seconds
Episode Artwork

Kama huna uhakika Yesu akikuita muda huu huna uhakika hakikisha leo unaokoka

Kama huna uhakika Yesu akikuita muda huu huna uhakika hakikisha leo unaokoka Wakati fulani tulisafiri na mzungu mmoja alikuwa ni mjerumani toka Arusha kwenda Dar es salaam. Aliombewa lift na mwenzake ili tusafiri naye, tukamuuliza je umeokoka akasema hapana. Yeye anamuabudu shetani na anatoka kanisa linalomuabudu shetani. Nikamwambia hamna kanisa la namna hiyo. Nikamuuliza alikuwa anasali kanisa gani akanitajia kanisa la Kikristo alilokuwa anaabudu kabla ya kuacha. Tukamuuliza tena kwa nini uliacha kwenda kanisani? Na akasema kanisa ni “very boaring” na kumepoa sana kanisani. Alisema huwa wanamtaja Mungu na sijawahi kumuona kanisani, lakini shetani anapojatwa huwa namuona. Wakati huo nilikiwa naendesha gari, nikamuuliza tena kuwa hapa tukipata ajali tukafa je utaenda wapi? akasema sijui. Nikamwambia sisi tukifa hapa tunaenda mbinguni. Nikamwambia huko ulikoenda siyo kuzuri maana walitakiwa kukueleza kuwa utaenda wapi baada ya dunia hii. Tulipofika Mombo nikawa naendesha gari huku naomba na kuangusha ngome katika akili yake. Baada ya hapo nikamwambia kuwa ukiwa tayari kama unataka kumpa Yesu maisha ili ukifa leo uende mbinguni utaniambia nisimamishe gari. Nikaendelea kuombea akili zake. Basi tulipofika Korogwe akasema Mwakasege simamisha gari namtaka huyu Yesu unayemsema. Nikapaki pembeni nikamuongoza sala ya Toba. Sasa nikamuuliza kuwa unaenda wapi? Akasema anaenda Zimbabwe. Maana nilijiuliza kuwa kwanini atoke Arusha asafiri kwa gari hadi Dar es Salaam halafu atafute ndege ndipo aende Zimbabwe?. Kama si Mungu kumpangia maana kamkimbia Yesu Ujerumani na kakamatiwa Tanzania. AMBA ZA SADAKA NA MAOMBI 👉🏼 https://goo.gl/7XcFiP MAOMBI YA KUOKOKA NA KITABU CHA HONGERA KWA KUOKOKA. 👉🏼 https://goo.gl/XKoJNB
8/12/20198 minutes, 40 seconds
Episode Artwork

Kumwamini Mungu kwa kumfuata Yesu Kristo (Sehemu ya Nne)

Tunapozungumza juu ya kumtumikia Mungu watu wengi sana hufikiria watu wachache tu yaani wahubiri, wachungaji, wainjilisti au wanaofanya kazi kanisani. Lakini kwenye Biblia inasema kila kiungo katika mwili wa Kristo kina nafasi yake na kazi yake kwa hiyo ni mtumishi wa Mungu. Inawezekana usihubiri, lakini pale ulipo ni mtumishi wa Mungu maana yake usimame katika kusudi lake ni kueneza Ufalme wake katika kazi ufanyayo. Hakikisha watu wanamjua Mungu maana Biblia inasema kila aliye mwana anao ushuhuda haisemi kila aliye mtumishi. Lakini pia kuna watu wengine ambao wanamtumikia Mungu bila wao kujua hata Israeli aliambiwa nimekufunga mshipi ingawa hukunijua ili wapate kunijua mimi ya kwamba hakuna Mungu kama mimi Kwa hiyo wakati Mungu anamchukua Israeli ili amtumie Israeli kujifunua kwa ulimwengu, Mungu anasema Israeli hakumjua. Kwa hiyo Mungu anaweza kukutumia wakati wewe humjui kwa sababu zake yeye, anaweza kujifunua wakati anaendelea kukutumia au anaweza kunyamaza. Maana Yesu anasema Ni nani basi yule mtumwa mwaminifu mwenye akili, kwa hiyo kwenye jambo lolote la kumtumikia Mungu, kwenye jambo lolote la kuishi hapa duniani, kati ya lengo mojawapo ambalo Mungu anategemea kila mtu awe nalo liwe ni lengo la kukutana na Yesu na kuishi naye milele Hivyo ni muhimu sana kuzungumza na waliokuzunguka kwa habari ya maisha yao na Yesu kabla ya kuondoka hapa duniani ndivyo Wathesalonike inavyotuambia 1 Wathesalonike 4:13-16 “Lakini, ndugu, hatutaki msijue habari zao waliolala mauti, msije mkahuzunika kama na wengine wasio na matumaini. Maana, ikiwa twaamini ya kwamba Yesu alikufa akafufuka, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye. Kwa kuwa twawaambieni haya kwa neno la Bwana, kwamba sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana, hakika hatutawatangulia wao waliokwisha kulala mauti. Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.” 1 Wathesalonike 5:1-2 “Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie. Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.” 1 Mambo ya Nyakati 12:32 “Na wa wana wa Isakari, watu wenye akili za kujua nyakati, kuyajua yawapasayo Israeli wayatende; vichwa vyao walikuwa watu mia mbili na ndugu zao wote walikuwa chini ya amri yao.” Anazungumzia juu ya kurudi kwa Yesu na maandiko yanasema kwa sababu hatujui siku wala saa basi tujiweke tayari, yaani tukae mkao wa kuwa tayari wakati wote.
7/24/20199 minutes, 48 seconds
Episode Artwork

Kumwamini Mungu kwa kumfuata Yesu Kristo (Sehemu ya Pili)

KUMWAMINI MUNGU KWA KUMFUATA/KUPITIA KWA YESU KRISTO. Ukisoma Luka 8:12 “Wale wa karibu na njia ndio wasikiao, kisha huja Ibilisi akaliondoa hilo neno mioyoni mwao, wasije wakaamini na kuokoka.” Pia Warumi 1:28 “Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa.” Ufahamu ulioko ndani ya akili zisizofaa zilifanya wamkatae Mungu. Kwa hiyo akili itafanya mtu amkubali au amkatae Mungu. 2 Wakorintho 11:3 “Lakini nachelea; kama yule nyoka alivyomdanganya Hawa kwa hila yake, asije akawaharibu fikira zenu, mkauacha unyofu na usafi kwa Kristo.” Shetani akitaka uache usafi na unyoofu wa Kristo, hashambulii roho yako kwanza; anashambulia fikira zako kwanza au kinachokusaidia kufikiri, yaani akili. Shetani alipotaka kufikia roho ya Adamu na Hawa alishambulia fikra zao, kwa hiyo akitaka kuzuia watu wasimwamini Yesu kama jinsi Mungu alivyomtuma, atashikilia fikira. Ukisoma 2 Wakorintho 4:3‭-‬4 “Lakini ikiwa injili yetu imesitirika, imesitirika kwa hao wanaopotea; ambao ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu.” Mathayo 22:36‭-‬37 “Mwalimu, katika torati ni amri ipi iliyo kuu? Akamwambia, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote.” Akimaanisha kuwa akili zako ziwe na namna fulani ziweze kushiriana na roho na imani la sivyo kumpenda Mungu wako kutapwaya mahali. 2 Timotheo 3:8‭-‬9 “Na kama vile Yane na Yambre walivyopingana na Musa, vivyo hivyo na hawa wanapingana na ile kweli; ni watu walioharibika akili zao, wamekataliwa kwa mambo ya imani. Lakini hawataendelea sana; maana upumbavu wao utakuwa dhahiri kwa watu wote, kama vile na upumbavu wa hao ulivyokuwa dhahiri.” Kinachofanya wapingane na kweli ya Mungu ni akili zao kwa sababu zimeharibika tofauti na kiwango Mungu anachotaka, na kwa sababu hiyo zile akili zinapingana na ile kweli na kusababisha kuwa mbali na imani na kukosa kufanya kazi na kushiriana kama zilivyokusudiwa kushiriana. Unaweza ukawa na msimamo mkali kabisa ukifikiri ni msimamo wa kiroho, kumbe ni akili zako zimekuwekea ugumu usielewe na usisogee. Tuangalie 1 Yohana 5:20 “Nasi twajua kwamba Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupa akili kwamba tumjue yeye aliye wa kweli, nasi tumo ndani yake yeye aliye wa kweli, yaani, ndani ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli, na uzima wa milele.” Kazi mojawapo ya akili ni kumjua Yeye Aliye wa Kweli. Kwa nini nimeanza na huo mfano? Ni kwa sababu watu wengi sana hawajajua ya kwamba Mungu aliweka hivi vitu viweze kufanya kazi pamoja. Nilishangaa sana nilipokuwa nikisoma Biblia na kufutalia uumbaji wa mwanadamu na zaidi pale Mungu aliposema na tumuumbe mtu kwa mfano wetu na akampa mwili, kwa sababu Mungu hana mwili kama tulio nao ni roho peke yake ambayo inaruhusiwa kuishi kwenye maeneo mawili kwa wakati mmoja bila shida. Mwanadamu aliruhusiwa na aliumbwa aweza kuishi katika ulimwengu wa kimwili na wa kiroho kwa wakati mmoja. Aweze kuishi katika ulimwengu wa kimwili, lakini aweze kuwasiliana na kuishi katika ulimwengu wa kiroho bila shida. Mungu alipokuwa anataka kushirikiana na sisi kutusaidia ilibidi atafute dada mmoja aitwaye Mariam apite kule ndani achukue mwili, na ndiyo maana Biblia inasema mwili nilikuwekea tayari la sivyo ingekuwa ngumu sana kutembea kama sisi na kufa pale msalabani, ilibidi lazima awe na mwili kama wetu. Maana maandiko yanasema kuna miili ya duniani na miili ya mbinguni. Asingeweza kutumia mwili wa mbinguni kuja kutusaidia, ilibidi lazima awe na mwili wa duniani na ndiyo maana Biblia inasema alivua utukufu wake ili aweze kuja duniani. Na Mungu alimuumba mtu kwa namna ambavyo hawezi kuishi katika kiwango ambacho Mungu alikikusudia bila Mungu na ndiyo maana tuliumbwa kwa mfano wake na kila kitu kingine kiliumbwa kwa mfano wa hicho kitu. Lakini mwanadamu peke yake ndiye ambaye alizuiwa asizae kwa mfano wake. Maana hatukuumbwa kwa mfano wa mwanadamu bali kwa mfano wa Mungu, lakini tukaitwa wanadamu ili tusizae mfano wa wanadamu bali tuzae mfano wa Mungu. Mwanadamu alipomkataa Mungu ule uzima wa Mungu na sura ya Mungu ndani viliondoka, maana alimkataa na akakubali roho ya upande mwingine ile roho ya giza kuja kutawala maisha yake.
7/19/20199 minutes, 48 seconds
Episode Artwork

Kumwamini Mungu kwa kumfuata Yesu Kristo (Sehemu ya Kwanza)

KUMWAMINI MUNGU KWA KUMFUATA/KUPITIA KWA YESU KRISTO. Hapa nilitaka uone katika ule mji Yesu alimpata mtu mmoja tu kwa lugha ya sasa tungesema “kwenye safari ya Yesu kuingia gharama ya kuvuka na boti kwenda kule na kufanya huduma alimpata mtu mmoja tu kwenye ule mji, na tofauti yao ilikuwa kwenye akili. Ingawa kwenye lile eneo wengine hawakuwa vichaa, haina maana kwamba akili zao zilikuwa huru hazijashikwa. Huyu Mgerasi kichaa alipofunguliwa alikuwa huru na ikawa rahisi sana kwa yeye kumfuata na kumhubiri Yesu, wenzake wote walimwambia Yesu aondoke kwao, lakini huyo aliyeponywa bado alikuwa ana ujasiri wa kurudi na kumhubiria huyo huyo Yesu waliyemfukuza. Ukisoma Mwanzo 2:7 “BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.” Ayubu 32:8 “Lakini imo roho ndani ya mwanadamu, Na pumzi za Mwenyezi huwapa akili.” Kwa hiyo akili iko ndani ya nafsi na ubongo uko ndani ya mwili. Kama katika uumbaji wa mtu, Mungu alitanguliza roho halafu akaleta mwili ndipo akaleta nafsi, kazi mojawapo ya nafsi ni kuwa kiungo, si tu cha mawasiliano kati ya roho na mwili. Lakini ukitaka kufikia roho kirahisi unapita kwenye nafsi, na ukitaka kufikia mwili kirahisi unapitia kwenye nafsi. Roho na mwili lugha zao hazielewani (roho inaenda kwa imani, mwili unaenda kwa milango ya fahamu (kuona, kugusa, kunusa, kuhisi kwa ngozi). Kwa hiyo nafsi imekaa hapo katikati, na akili imekaa hapo katikati. Biblia inajitafsiri yenyewe, ukikuta mstari huu huuelewi, unakuta mahali pengine neno hilo limefafanuliwa.
7/19/201910 minutes, 5 seconds
Episode Artwork

Kumwamini Mungu kwa kumfuata Yesu Kristo (Sehemu ya Tatu)

Kwa hiyo tangu wakati ule kuna vitu ambavyo alivyokuwa anafanya moja kwa moja vinazaa tena mfano wa kile kitu alichobeba. Sasa unaweza ukaelewa kwa nini katika kipindi hiki cha Agano jipya ni lazima tuzaliwe kwa mara ya pili. Maandiko yanatuambia ndani yake tunaishi, tunakwenda na kuwa na uhai wetu na Biblia inatuambia tutaishi kwa imani Ni imani ya namna gani? Waebrania anasema Waebrania 11:6 “Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.” IMANI YA KWANZA NI HII:- PASIPO IMANI HAIWEZEKANI KUMPENDEZA; KWA MAANA MTU AMWENDEAYE MUNGU LAZIMA AAMINI KWAMBA YEYE YUKO Yaani usiishi kama vile Mungu hayupo. Kwenye Kiswahili cha kawaida tunahiita Uchaji Kwenye tafsiri nyingine ya kiingereza inaitwa hofu ya Mungu The fear of God. Kujua ya kwamba Mungu yupo. Kwa sababu ile tu kujua ya kwamba Mungu yupo inatosha kubadilisha na kuweka msimamo wako na malengo yako kwa namna ambavyo unajua Mungu yupo. IMANI YA PILI NI HII:- KILA AMWENDEAYE MUNGU LAZIMA AAMINI KWAMBA YEYE YUKO, NA KWAMBA HUWAPA THAWABU WALE WAMTAFUTAO Kwa nini tunamtafuta? kwa sababu dhambi ilitutenga naye. AINA NYINGINE YA IMANI NI KWENYE KITABU CHA Waebrania 11:1 “Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.” Kwa sababu dhambi ilipoingia ilituvurugia mawasiliano yetu ya kawaida na vitu visivyoonekana na ulimwengu wa roho. Maana ilikuwa ukienda kwenye ulimwengu wa roho ni au Mungu ajifunue kwako la sivyo utakutana na ulimwengu wa roho wa ulimwengu wa giza na ndiyo maana wanadamu ni wepesi sana kushabikia vitu vya ulimwengu wa giza kuliko vile vya ulimwengu wa nuru, kwa sababu hivyo vya giza ndiyo mazingira tuliyonayo. Shetani anajiita mungu wa dunia hii na katengeneza mazingira ambayo ni kitu cha kawaida huoni watu wakishtuka watu wakienda kwenye nguvu za giza, lakini watashtuka wakisikia kwenye familia mtu akiokoka. Imani inapokuja katika Kristo Yesu au katika Neno la Mungu kazi yake mojawapo ni kukutengenezea kitu mbele yako lengo ni kitu kilichopo mbele yako ambacho unataka kukifika, na Mungu asingetaka uende na malengo yoyote unayotaka Kwa sababu Yeremia anasema Yeremia 29:11 “Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho.” Tafsiri nyingine anasema “ninajua mpango niliowapangia mimi asema Bwana ni mpango wa kuwafanikisha na kuwapa tumaini katika siku zenu za usoni” Kwa hiyo Mungu analo alilokuletea duniani, huji duniani halafu unatafuta ambalo Mungu alitaka ufanye, unakuja duniani kwa sababu lipo tayari na unatakiwa ulifanye wakati huu. Na Mungu ndiye anajua. Kwa hiyo kama unataka kulijua hilo kusudi, mjue Mungu kwanza. Watu wanataka kujua Mungu alichowapa wafanye lakini hawataki kumjua Mungu. Biblia inasema mjue sana Mungu ili uwe na amani ndivyo mema yatakavyokujia Kwa hiyo kuna ile imani ya kuwa na kitu unachokitarajia, kunakuwa na malengo kwenye maisha ya kwako na hayo malengo saa hii unakuwa huyaoni kwa jinsi ya nje lakini imani inakusaidia uyaone na unakuwa na uhakika ya kwamba Mungu yupo pamoja na wewe kwa sababu siyo imani uliyoiokota mahali, bali ni imani inayotokana na Neno la Mungu kiasi ambacho kile unachokikusudia, kile unachojiwekea malengo hakiko nje ya Neno la Mungu bali kiko kwenye maisha aliyokutengenezea. Na Mungu aliweka ya kwamba Imani na Akili na Mwili vifanye kazi pamoja. Kwa lugha rahisi zaidi ni kwamba aliumba roho, nafsi na mwili vifanye kazi pamoja. Kwa hiyo katika roho Neno la Mungu likija unapokea Imani, na katika nafsi Neno la Mungu likija unapewa kuelewa ndiyo maana BIblia inasema akawafunulia akili zao wapate kuelewa na maandiko Roho haihitaji kuelewa ili kumfuata Mungu, yenyewe inahitaji kuamini na ikiisha kuamini inasonga mbele lakini akili inahitaji kuelewa, kwanini? Ili iwe na nafasi ya kuuelewesha mwili kwa sababu kufuatana na Biblia mwili hauna mpango wa kwenda mbinguni. Usifikiri ni kitu chepesi sana kwa sababu unapokuwa mtendaji wa Neno inamaanisha mpaka mwili uweze kuhusika, vinapoanza kushindana kati ya imani yako na unachofikiri na unachotaka kufanya uwe na uhakika malengo yako huwezi kuyafikia, yatabaki tu kwenye makaratasi na moyo wako maana upinzani mkubwa unaanza ndani yako na shetani anajua mahali pa kukamata ni kwenye akili. Na ndiyo maana kama unataka kumjua Mungu na kumfuata Yesu na neno lake jifunze kuombea akili zako. UHUSIANO WA KUMTUMIKIA MUNGU NA KURUDI KWA YESU (Sehemu ya Kwanza) Mathayo 24:45-51,44 “Ni nani basi yule mtumwa mwaminifu mwenye akili, ambaye bwana wake alimweka juu ya nyumba yake, awape watu chakula kwa wakati wake? Heri mtumwa yule, ambaye bwana wake ajapo atamkuta akifanya hivyo. Amin, nawaambieni, atamweka juu ya vitu vyake vyote. Lakini mtumwa yule mbaya akisema moyoni mwake, Bwana wangu anakawia; akaanza kuwapiga wajoli wake, na kula na kunywa pamoja na walevi; bwana wake mtumwa huyo atakuja siku asiyodhani, na saa asiyojua, atamkata vipande viwili, na kumwekea fungu lake pamoja na wanafiki; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno. Kwa sababu hiyo ninyi nanyi jiwekeni tayari; kwa kuwa katika saa msiyodhani Mwana wa Adamu yuaja.” Tunapozungumza juu ya kumtumikia Mungu watu wengi sana hufikiria watu wachache tu yaani wahubiri, wachungaji, wainjilisti au wanaofanya kazi kanisani. Lakini kwenye Biblia inasema kila kiungo katika mwili wa Kristo kina nafasi yake na kazi yake kwa hiyo ni mtumishi wa Mungu. Inawezekana usihubiri, lakini pale ulipo ni mtumishi wa Mungu maana yake usimame katika kusudi lake ni kueneza Ufalme wake katika kazi ufanyayo. Hakikisha watu wanamjua Mungu maana Biblia inasema kila aliye mwana anao ushuhuda haisemi kila aliye mtumishi. Lakini pia kuna watu wengine ambao wanamtumikia Mungu bila wao kujua hata Israeli aliambiwa nimekufunga mshipi ingawa hukunijua ili wapate kunijua mimi ya kwamba hakuna Mungu kama mimi Kwa hiyo wakati Mungu anamchukua Israeli ili amtumie Israeli kujifunua kwa ulimwengu, Mungu anasema Israeli hakumjua. Kwa hiyo Mungu anaweza kukutumia wakati wewe humjui kwa sababu zake yeye, anaweza kujifunua wakati anaendelea kukutumia au anaweza kunyamaza.
7/19/201910 minutes, 13 seconds
Episode Artwork

Tufanye maombi na kuombea akili zetu na kutuondoa katika kushikwa na shetani! Omba sasa

Baada ya sala na mafundisho ya Mwalimu Christopher Mwakasege changia huduma ya Mana Ministries iweze kuendelea, kukua na kufikia watu wengi zaidi ndani na nje ya nchi. NAMNA YA KUPATA KANDA, CDs & DVDs BONYEZA HAPA 👉🏼 https://goo.gl/xrSwmN NAMBA ZA SADAKA NA MAOMBI 👉🏼 https://goo.gl/7XcFiP MAOMBI YA KUOKOKA NA KITABU CHA HONGERA KWA KUOKOKA. 👉🏼 https://goo.gl/XKoJNB
7/18/20199 minutes, 38 seconds
Episode Artwork

Weka akiba mapema ikusaidie pale utakapo staafu

Maana akili zako zinakuwa zimebanwa kabisa unapata pesa na unazitumia kienyeji kienyeji tu. Ili uweze kuelewa tafuta watu waliostaafu. Wengi sana wana maisha mabaya na ni wachache sana wana maisha mazuri, kwa sababu wengine walikuwa na maisha mazuri sana walipokuwa kazini. Walikuwa na magari na nyumba kumbe ni za shirika au kampuni ambayo anafanyia kazi lakini sio vya kwake. Maana wakati wa zamani wafanyakazi walikuwa wanapewa kila kitu hadi furniture za ndani, ukiwaona utafikiri ni vya kwao kumbe sio vyao ni vya shirika akifukuzwa kazi au hiyo kazi ikiisha ndipo utaona namna maisha yake yanavyobadilika kabisa. Tulikuwa mkoa mmoja, tulikuta mchungaji ambaye alifariki ghafla akiwa kwenye safari ya kikazi. Aliacha watoto wake sita, mke wake na watoto wa ndugu zake sita. Kwa hiyo nyumbani kwake kulikuwa na watoto kumi na mbili. Mchungaji mpaka anakufa alikuwa hana nyumba. Baada ya mazishi na baada ya miezi mitatu kupita wazee wa kanisa na baadhi ya Viongozi wa lile kanisa wakimwendea yule mke wa mchungaji aliyefariki.Wakamuambia kuwa mama tunamshukuru Mungu kwa ajili yamume wako maana kwa kweli tuliona mkono wa Mungu juu yake sijui kwanini Mungu alimchukua mapema. Walianza mbali kuanza kuongea nae, na walisema mama unajua kilichotuleta ni kuwa mambo lazima yaende na Mungu katupatia mchungaji mwingine. Sasa tunahitaji hii nyumba ili aje aishi hapa. Yule mama alikuwa hana mahali pengine pa kwenda yule mama alitusimulia yeye mwenyewe maana anasema baada ya hapo alianza kulia na akapata pressure na akaugua muda mrefu sana. Ile kazi aliyokuwa anafanya alifukuzwa maana hakuonekana kazini muda mrefu sana kwa sababu ya kuumwa. Je unataka kwenda kiroho na future ya familia????, unakufa hujaacha mambo ya familia kikaa sawa, ukiondoka unawachia mama na watoto mzigo mzito sana.
7/17/201910 minutes, 21 seconds
Episode Artwork

Kutumia Ubongo na akili kufanya maamuzi ya chanzo na matumizi ya pesa zako

UBONGO UNATAKIWA UKUSAIDIE KUWA NA MIPANGO YA KUPATA PESA LAKINI AKILI INATAKIWA ZIKUSAIDIE KUAMUA JUU YA CHANZO CHA KUPATA PESA NA KUAMUA MATUMIZI YA PESA HIZO Kazi mojawapo ya akili ni kutusaidia kupambanua mema na mabaya kwa jinsi ya Ki-Mungu ili tuweze kuchagua mema na kuacha mabaya. Biblia inatuambia kuwa akili zao kwa kutumiwa. haijasema kwa kutegemewa bali ni kutumiwa. Biblia imekataza kutegemea akili bali tunatakiwa tumtegemee Mungu. Shetani akitaka kuvuruga maisha yako atakamata akili zako maana ubongo unaweza kuwa na mipango mizuri sana ya kupata pesa lakini akili zako zisiwe vizuri katika kuangalia chanzo na matumizi ya pesa zako. Maana unaweza ukawa na mipango mizuri sana mbele ya watu au nchi lakini inaweza isikupe hela. Maana unaweza pata hasa sadaka ya shukrani ya kutoa jumapili katika hizo pesa zako. Lakini chanzo chako hakiko sawa maana kumbe hizo pesa umevunja benki mahali ukaiba. Fikiria mtu ambaye kaenda shule vizuri na kawa mhasibu mzuri na anapata mshahara mkubwa sana. Kitu cha kwanza anachofanya akiwa kazini anaanza kuiba. Sasa hapo kapata kazi kwa kutumia ubongo lakini akili zake haziko kazini na kwa sababu hiyo shetani anazitumia kumfanya aibe. Maana kama kaenda chuo na kapata cheti kwamba kasomea masuala ya accounting na Finance. Sasa badala ya kwamba kwa kuwa kasoma vizuri basi atumie ujuzi wake kuandika vizuri katika kutunza kumbu kumbu vizuri yeye anaandika asionekane kama kaiba pesa kumbe anaibia shirika au kampuni anayofanyia kazi. Lakini watu wa namna hii wanasema ni wizi wa kutumia akili. Lakini akili zimetumika vibaya na kumfanya mtu kwenda kuiba. Unahitaji kuwa na akili nzuri ambazo zinakuelekeleza kuwa hii njia ni sahihi lakini hii ni mbaya. Akili inakusaidia juu ya kutumia pesa hasa katika kuweka akiba. Mwanzo 41: 33-36 Basi, Farao na ajitafutie mtu wa akili na hekima amweke juu ya nchi ya Misri. Farao na afanye hivi, tena akaweke wasimamizi juu ya nchi, na kutwaa sehemu ya tano katika nchi ya Misri, katika miaka hii saba ya kushiba. Na wakusanye chakula chote cha miaka hii myema ijayo, wakaweke akiba ya nafaka mkononi mwa Farao wakakilinde kuwa chakula katika miji. Na hicho chakula kitakuwa akiba ya nchi kwa ajili ya miaka hiyo saba ya njaa, itakayokuwa katika nchi ya Misri, nchi isiharibike kwa njaa. Yusufu alimwambia Farao atafute mtu wa akili na hekima ili akae juu ya Misri aweze kuweka akiba kwa ajili ya kipindi cha njaa. Mithali 30: 24-25 Kuna viumbe vinne duniani vilivyo vidogo; Lakini vina akili nyingi sana. Chungu ni watu wasio na nguvu; Lakini hujiwekea chakula wakati wa joto. Chungu ni watu wasio na nguvu, sasa haina maana hawa ni watu ila inapofika katika suala la kuweka akiba wana akili kama za watu. Lakini ukweli ni kuwa chungu ni aina ya siafu au sisimizi. Katika ; Mithali 6:6-11 Ewe mvivu, mwendee chungu, Zitafakari njia zake ukapate hekima. Kwa maana yeye hana kiongozi, Wala msimamizi, wala mkuu, Lakini hujiwekea akiba ya chakula wakati wa jua; Hukusanya chakula chake wakati wa mavuno. Ewe mvivu, utalala hadi lini? Utaondoka lini katika usingizi wako? Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, Bado kukunja mikono upate usingizi!Hivyo umaskini wako huja kama mnyang'anyi, Na uhitaji wako kama mtu mwenye silaha. Kuna umasikini wa kukosa akiba na si umasikini wa kukosa pesa maana watu wengi ndio wamekwama hapa. Shida yake iko kwenye akili maana Mungu kaweka akili ifanye maamuzi ya kuweka akiba. Sisimizi huwa wanakusanya chakula wakati wa hari/kiangazi ili kitumike wakati wa baridi. Kama hujakaa nchi za baridi unaweza usielewe maana unaweza fikiria baridi kama ile ya mwezi wa sita tu.Sasa ile baridi kwa msemo wa mjini tungesema hiyo ni cha mtoto. Sasa ukienda nchi za Kaskazini au kusini mwa dunia. Kuna baridi kali sana huwa inaanza mwezi October hadi Machi. Kunakuwa na baridi kali sana maana huoni hata sehemu ya ardhi hasa kama unapita na ndege isipokuwa barabara tu ambapo huwa wanakwangua. Baridi inashusha barafu sana maana inaweza shusha hadi dari ya nyumba maana ni nzito sana. Maana hata gari likiachwa nje huwa linafunikwa na barafu kabisa hadi kesho unaweza usilione maana linakuwa limefunikwa kabisa. Maana huwa wanachimba na spedi ili kuweza kulitoa gari lilipofunikwa na barafu. Sasa unaweza ukaelewa hawa wadudu wanakaa kipindi chote cha baridi wakiwa hai. kwa hiyo wanajua kuna kipindi cha kukusanya, maana wanajua kabisa hawatakiwi kula chakula chote maana wanajua kuna msimu wa njaa. Biblia inaposema hawana akida maana yake hakuna mtu wa kuwasimamia au hawana serikali ya kuilalamikia kuwa wanapita kipindi cha njaa kwa hiyo wanahitaji msaada. Wasipoweka akiba ni kwa hasara yao maana ukifika wakati wa baridi watakosa chakula na mwishowe watakufa. Watu wengi ambao hawana akiba sio kwamba hawana hela bali ni kuwa hawajui mgawanyo na kinachogawanya pesa za sasa na za kesho ni akili, sio roho. Ukitaka kukwama sasa hapo jaribu kwenda kiroho kuweka akiba, ujue lazima utakwama tu. USHUHUDA. Kuna rafiki yetu mmoja alikuwa anakula kila kitu anachopata. Alikuwa anasema siweki akiba maana sitaacha mtu hapa Duniani. Kwa hiyo alikuwa akipata kila chochote anakula kila kitu hata hatunzi akiba maana alikuwa anasema wasije watu wakagombania siku tukifa maana itakuwa shida sana. Kwa hiyo hata kama kapata zaidi basi kilichozidi alikuwa anatoa sadaka. Siku moja walipata ajali yeye na mke na watoto wao wawili wote walikufa. Huyu ndugu japo walikufa wote siku moja yaani yeye na familia yake lakini alikuwa anaishi kiroho, lakini haitakiwi uishi hivyo maana lazima ujue kuna kesho, kuna watoto watabaki kwa hiyo tumia akili yako vizuri kuweka akiba. Pia katika kuweka akiba weka akiba kwa utaratibu ambao Mungu kakupa.Wamisri walipoambiwa waweke akiba ya nafaka wao waliweka akiba za pesa na za wanyama. Sasa akiba yao iliishia baada ya muda mfupi na haikuwa na msaada kwao maana baada ya mwaka mmoja walimaliza kika kitu. Walijiuza wao na ardhi yao na haikuwa wakiwatosha. Maana bado walikuwa na miaka minne mbele na hawana kitu. Tuje kwako wewe je akiba ambayo unayo kama iko benki au mahali popote unapojua wewe, jaribu kufikiria kama huna kipato chochote kuanzia sasa na huna msaada wowote, je hiyo hela uliyonayo itakufikisha wapi? Ndipo utagundua kuwa hata mwezi humalizi ndipo utajua maisha yako yako hatarini kiasi gani. Biblia inaita umasikini wa kukosa akiba maana sio umasikini wa kukosa kipato. Shetani akitaka kukubana ili ukose akiba, atabana fikra zako wakati wa kiangazi ili usiweze kuweka akiba. Atabana akili zako uko kazini wakati huo unapata mshahara wako vizuri na unafikiri kuwa hiyo kazi haitaisha na hata wewe hukumbuki kuweka akiba. Atabana wakati biashara yako inaenda vizuri ili usikumbuke kuweka akiba wakati biashara inaingiza pesa nyingi, wewe hukumbuki hata kuweka akiba maana unajua huo mzunguko utakuwepo na kesho. Kumbuka kuwa kuna kipindi cha miaka saba ambacho kinaweza kikaja na shida, lakini wakati wa unono wa miaka saba unabanwa hata hukumbuki kuna kipindi cha njaa kinakuja. Hapo ndipo shetani anabana watu wengi sana maana unakuwa na pesa lakini unabanwa kuweka akiba. Hata ukijaribu kudunduliza unakwama kabisa. Shetani akitaka kukubana atakubana wakati una kipato kizuri usiweke akiba kwa ajili ya wakati ambao hutakuwa na kipato hicho tena.
7/16/20199 minutes, 46 seconds
Episode Artwork

Jifunze kukaa na mkeo kwa akili na si kiroho, jifunze sasa!

Biblia haisemi wanaume tukae na wake zetu kiroho, kwa hiyo usijaribu kukaa na mke wako kiroho, kaa nae kwa akili. Ndani ya akili hizo Mungu atakupa neema ya kumsaidia kumpa heshima anayostahili. Lakini kuona ile nafasi kwa jinsi ya mwili ni chombo kisichokuwa na nguvu lakini katika ulimwengu wa roho wana nguvu kuliko sisi! Kwanini Mungu ameumba jambo jipya mwanamke atamlinda mwanaume wanawake ni walinzi wazuri sana katika ulimwengu wa roho, wana nguvu za kiroho kuliko wanaume lakini inapokuja kwenye maisha ya kawaida Biblia inasema mpe heshima maana ni kiumbe dhaifu. Unaweza ukampenda mke wako lakini usimheshimu, Biblia inasema kama warithi pamoja wa neema,je huwa unamshirikisha mke wako kwa kiwango gani kitu ulichonacho? Kuna watu ambao vitu vyao ni siri kiasi kwamba hata akifa ni shida kujua hata alikuwa na account wapi, alikuwa pesa kiasi gani, viwanja vingapi! Hata mke hajui na siku akifa anaanza kuhangaika kama mtu mwingine. Tito 2:3-5 Vivyo hivyo na wazee wa kike wawe na mwenendo wa utakatifu; wasiwe wasingiziaji, wasiwe wenye kutumia mvinyo nyingi, bali wafundishao mema; ili wawatie wanawake vijana akili, wawapende waume zao, na kuwapenda watoto wao;na kuwa wenye kiasi, kuwa safi, kufanya kazi nyumbani mwao, kuwa wema, kuwatii waume zao wenyewe; ili neno la Mungu lisitukanwe. Biblia inatuambia wanawake watu wazima wamepita mahali wameona umuhimu wa akili ndio maana biblia inasema wasaidieni hawa wanawake vijana watieni akili.Mwanamke anatumia akili kumpenda mume wake na mwanaume anatumia akili kumpa heshima mke wake. Hapo roho haitajwi katika kupenda wala kumpa mke heshima bali ni akili inatumika. Biblia inasema na kuwapenda watoto wao, maana unaweza ukawapenda watoto yatima lakini wa kwako usiwapende.Haitoshi tu kusema unawapenda watoto maana unaweza ukasahau kuwapenda watoto wako mwenyewe. Ndio maana biblia inasema wanawake wawatie wanawake vijana akili za kuwapenda watoto wao na waume zao, kuwa wenye kiasi, na kuwa safi. Kwa hiyo mwanamke akiwa mchafu shida ni akili zake. Kwa hiyo kama pepo limemfanya kuwa mchafu ina maana limeshika akili zake, maana inatakiwa akili zitumike ili kumfanya kuwa safi. Mwanamke anatakiwa kufanya kazi nyumbani mwake. Maana anaweza fanya kazi kwingine lakini nyumbani mwake asifanye kazi. Pia wanawake wanatakiwa kuwa wema na kuwatii waume zao wenyewe. Kuna baadhi wanawake wanawatii sana wachungaji zao kuliko waume zao, maana si vibaya kumtii mchungaji. Lakini kumbuka mume akimfukuza huyo mke wake, mchungaji hawezi kumuoa. Pia mke wa mchungaji nae akikaa vizuri kwenye nafasi yake endapo akienda mwanamke aliyefukuzwa na mume wake akaenda kwa mchungaji kuomba msaada, atamuuliza “ unaenda wapi kwani huna kwenu?”. Hata akijieleza kuwa kaenda ili kupata ushauri, maana wanaweza mvumilia kwa siku chache hata kama watampa hifadhi ila baada ya muda mfupi watamuuliza kwanini haendi kwao kama kafukuzwa na mume wake? Maana hatakiwi kukaa tena kwa mchungaji wake.
7/15/201910 minutes, 4 seconds
Episode Artwork

Ubongo unaona matatizo akili inaona fursa kwenye hayo matatizo

1 Mambo ya Nyakati 12:32 “Na wa wana wa Isakari, watu wenye akili za kujua nyakati, kuyajua yawapasayo Israeli wayatende; vichwa vyao walikuwa watu mia mbili na ndugu zao wote walikuwa chini ya amri yao.” Nataka uone hapa anaposema walikuwa watu wenye akili za kujua nyakati na kitu cha kufanya kwenye nyakati Kwanini? Kwa sababu ukisoma kile kitabu cha Mhubiri; Mhubiri 3:1-2 “Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu. Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung'oa yaliyopandwa;” Mungu alipanga vitu viende kwa muda na katika huo muda kuna vitu ambavyo tunatakiwa kufanya. MFANO Mungu alipomuumba mwanadamu pamoja na umuhimu wa magari hakutuumbia magari, na kwa sababu hiyo mwanadamu alipozaliwa na kuanza kutembea huku duniani kukosekana kwa barabara hakukuwa tatizo la kimaendeleo kwa nyakati zile, ubongo ulikuwa unaona kabisa kwamba hakuna barabara na akili ilikuwa inasema huna shida nayo. Lakini ikafika mahali muda unadai vitu viende kwa speed ndipo maswali ya usafiri yakaanza kuja na ndipo vikaja vyombo vya usafiri ili kurahisisha usafirishaji na mawasiliano na kurahisisha maendeleo kwenda kwa haraka. Sasa ilipofika mahali pa namna hiyo ubongo unapoona magari halafu hauoni barabara basi wenyewe (ubongo) unasema hili ni tatizo akili inasema hii ni fursa. Kwa hiyo ukitumia ubongo bila kutumia akili utalalamika.Ukitumia ubongo na akili utatafuta majibu ya changamoto na tatizo hilo. Ukiumwa jino kwako wewe unayeumwa jino ni tatizo lakini kwa daktari ni fursa. Ukiona garage zinajengwa wameona magari yanaharibika au wanatafuta fursa. Kama akili ikiwa kazini tafsiri ya vitu vilivyoko kwenye nyakati zilizoko zinakuwa tofauti kufuatana na nyakati. Ndio maana Mungu aliwaweka wana wa isakari wenye kujua nyakati na mambo yanayotakiwa yafanyike kwenye hizo nyakati nao walikuwa 200 na walikuwa viongozi wa ndugu zao. Mtu anayeweza kufikiri kesho yako kabla kesho haijafika uwe na uhakika atakuwa kiongozi wako. Mvua inanyesha unatafuta mwamvuli zamani hakukuweko miamvuli, mvua inanyesha unatafuta mwamvuli zamani tulikuwa tunatumia majani ya migomba lakini kuna mtu akafikiri akaona jinsi ambavyo mvua ikiisha unavyohangaika kutupa lile jani akafikiri kitu cha kujifunika ili mvua ikiisha anajifunika na kila alichofikiri unakilipia. Mungu alijua kabisa ili mwanadamu aweze kuishi vizuri anahitaji masaa 8 kati ya 24 na ukilimbikiza madeni ya usingizi utakuta unakosa utulivu na macho yanashindwa kuangalia vizuri, baada ya muda utaanza kupata shida ya kula chakula, sasa kama usingizi ulikuwa wa muhimu namna hii kwanini Mungu hakutengeneza kitanda! Na ukiangalia ⅓ ya maisha ya Mwanadamu anatumia kitandani kwa hiyo hii inamaanisha ni sehemu muhimu sana. Kwanini Mungu alipotuumba asingetengeneza na kitanda ni kwa sababu alitupa akili kwamba tuamue tunalala chini au tunatengeneza kitanda ni juu yetu. Tulienda hoteli moja kule Washington DC na tulikuwa kwenye msafara wa viongozi fulani miaka kadhaa iliyopita tukapewa chumba. Tukakitazama kile chumba na kitanda chake na tukakuta vitu vimewekwa pale mezani kwa hiyo tukaamua kuvisoma tukashangaa kumbe ni button za kukusaidia unataka kulalaje! Kwetu ukitaka kulala kichwa juu unaweka mto ukitaka kulala flat unaondoa mto wenzetu wameondoa hiyo shida ni unabonyeza tu button na kitanda kina ji adjust chenyewe. Lakini uliza bei ya chumba! Ni ghali mnoo. Nilienda Canada wakati wa baridi na nilipolalamika kuna baridi wakanipeleka kwenye chumba na chumba wameki balance hali ya joto na kuna blanket linatumia umeme. Nikaona amenyanyua blanket akavuta wire akaenda kwenye soketi ya umeme akachomeka halafu akawasha umeme halafu akaniambia ingia hapo ulale nikakataa! Walipoona nimeshtuka namna hiyo yule mwenyeji wangu akaingia akajaribu akaniambia si unaona mimi sijapata shock hamna shida! nikamwambia aaa wapi! Sasa katika shida yote ile walitafuta kurahisisha maisha akili na ndio maana akili zao zimeingia kazini. Wakati wewe unalalamika baridi wao wanaishi kwa sababu akili zao zinafanya kazi. Mahali wewe unalalamika wenzio wanajikita katika kutafuta fursa.
7/14/201910 minutes, 4 seconds
Episode Artwork

Sio swala la kuishi maisha marefu, ni swala la kuishi kwenye mapenzi ya Mungu

Unaweza ukawa unafurahia biashara uliyonayo na kufikiri kwamba umefika lakini Mungu ana kitu kikubwa kuliko unachofikiri. Ila hujajua kwamba huko ndani yako kuna kitu gani kimekaa na kwanini ndani yako unaona ndoto kubwa au unaona hujaridhika mahali ulipo kumbe Mungu anajaribu kukusukuma kukuonyesha kwamba ndani yako amekuwekea kitu kikubwa kuliko unacho fikiri. Hivyo usitosheke na mahali ulipo kisukume na usonge mbele na ukimwendea Mungu atakuonesha mahali unapotakiwa kuwa. Mungu alimpa Yusufu miaka 14 ya kutumia zile akili. Na ndiyo maana si suala la kuishi maisha marefu ni suala la kuishi katika mapenzi ya Mungu. Kuna wengine wanaishi maisha marefu na maisha yao hutaki hata kuyasikia, maana ni hasara tu mpaka kwa udongo. Lakini kuna wengine wana maisha mafupi kama ya Yesu, maana yeye alikufa kabla ya kufikisha miaka 40 na ni miaka 3 ndiyo iliyomleta hapa duniani miaka mingine unaona wakiandika habari zake kwa uchache sana. Miaka yake 3 ilibadilisha kila kitu na kuweka alama ambayo shetani hawezi kufuta. Sijajua Mungu amekupa mtu wa namna gani, au kwamba Mungu amekubebesha akili za namna gani ila ninachojua akina Yusufu wako tena yawezekana ni wewe. Wakati ukifika haijalishi uko jela au umesingiziwa Mungu atakutoa tu huko, ikifika saa ya kwako Mungu atatengeneza njia tu hata kama hakuna njia na kukufikisha mahali kila mtu atakutazama na kusema kama si Mungu aliyekuwa pamoja naye huyu mtu na aseme sasa. Na ndiyo maana Yusufu pamoja na kulia alipowaona ndugu zake hakuwa na sababu ya kuwachukia na kuwakasirikia alijua ya kwamba kama si Mungu wasinge fika pale na yeye asingefika pale. Kwa hiyo ukiona watu wanakuchukia na kukupiga vita njiani wakati unasonga mbele huhitaji kuwakasirikia wewe songa mbele maana hao hao wanaokuchukia leo kesho watakuja kukuomba mkate. Kwa hiyo ukiwa na akili kubwa usishindane na vidogo. Usiwe na muda wa kupoteza kwenye vitu ambavyo vinakuletea hasara tu. Nilikuambia akili sio ubongo akili iko ndani ya nafsi na ubongo uko ndani ya mwili lakini Mungu aliviumba vifanye kazi kwa pamoja kwa kushirikiana.
7/13/20199 minutes, 46 seconds
Episode Artwork

Haijalishi unapitia hali gani na upo kwenye kipindi gani, Mungu yuko pamoja nawe

Mtu aliyekuwa anatakiwa kwenye hii nafasi alitakiwa awe ana akili ya miaka 14 kusaidia Misri na nchi za jirani. Alitakiwa awe ana hekima pamoja na Roho wa Mungu ili kuweza kukamilisha jukumu hilo. Yusufu aligundua kuna kitu Farao alitakiwa akitolee nafasi (position) kwa sababu anaweza patikana mtu mwenye akili lakini asiwe na mahali pa kutumia akili zake. Kuna watu wana akili lakini hawana hekima na wengine wana hekima akili hawana. Yusufu alikuwa na hivyo vyote pia alikuwa na Roho wa Mungu ndani yake. Kwa maana hiyo Mungu alimpa nafasi ili aweze tumia akili, hekima na Roho ya Mungu iliyokuwa ndani yake katika kufanya alichotakiwa kufanya kwa miaka 14. Mwanzoni kabisa Yusufu aliotea ndoto akiwa na miaka 17 lakini alipewa kuwa waziri mkuu akiwa na miaka 30, kwa hiyo miaka 13 ilimtesa kufukia mahali pa kuweza kutumika miaka 14. Kwa sababu alipitia wakati mgumu sana miaka hiyo 13 maana Mungu alimleta duniani kwa kazi hizo kubwa. Moja ya kazi ni kuhakikisha ile miaka 14 pale Misri akili zake zinatumika sawasawa kwa sababu alisema Mwanzo 45:7‭-‬8 “Mungu alinipeleka mbele yenu kuwahifadhia masazo katika nchi, na kuwaokoa ninyi kwa wokovu mkuu. Basi si ninyi mlionipeleka huku, ila Mungu; naye ameniweka kama baba kwa Farao, na bwana katika nyumba yake yote, na mtawala katika nchi yote ya Misri.” Maana yake amekuwa na akili iliyomfanya kuwa baba kwa Farao mahali ambapo kwa jinsi ya kawaida isingewezekana pia akawa baba kwa taifa la Misri na kwa ndugu zake. Yusufu ndoto (vision) yake ilikuwa ya contract ya miaka 14. Lakini alifanya vizuri kiasi ambacho hakustaafishwa baada ya muda wake kuisha bali aliendelea na kazi mpaka alipo kufa. Kumbuka Yusufu alipewa akili ya kusaidia ndugu zake lakini ndugu zake walimkataa hata alipoenda kuwapelekea chakula walipomwona walimkasirikia wakaanza kupanga kumu ua. Sasa fikiria walitaka kuua akili ya namna gani kwa kubebeshwa kitu cha aina gani. Kwa hiyo ili wasimuue wakakubaliana kumtumbukiza kwenye kisima kisicho na maji halafu wakafikiria tena kuwa wamuuze kama mtumwa bila kujua thamani ya akili iliyokuwa inauzwa. Waishmaeli nao wakaja kumuuza kwa Potifa na Potifa baadae akamtazama akagundua Yusufu ana baraka fulani na sio akili tu. Potifa akamweka Yusufu kuwa kiongozi wa kila kitu nyumbani kwake. Aliposhindwana na mke wa Potifa akaishia jela, sasa fikiria ni akili gani ambayo ilikuwa imefungwa jela. Kuna wengine wamefungwa jela (jela hizi za kawaida kwa makosa halali au kwa kusingiziwa/kuonewa) na wana akili kama ya Yusufu. Pia mkuu wa jela akagundua baraka zilizokuwa juu ya Yusufu na kumpa cheo. Naye Yusufu akamsaidia mtu mkubwa sana katika taifa la Misri kwa kumtafsiria ndoto yake na akamwambia akirudi kazini kwake amkumbuke ili aweze toka jela. Lakini yule mtu alimsahau kwa hiyo Yusufu alisahauliwa jela miaka miwili. Ninaposoma hizi habari huwa namshangaa sana Mungu. Inawezekana umesahauliwa huna nafasi yoyote, huna kazi lakini hujui akili uliyobeba na inawezekana hata waliokuzunguka hawajui akili uliyobeba.Maana unaweza ukawa na upako lakini kuna watu wanaojaribu kutafuta kukuua na Mungu amenyamaza. Unaweza ukawa ndani ya birika na ndugu zako wakakuchukia kabisa. Usije ukafikiri Mungu amekuacha maana nguvu za Mungu ziko pamoja na wewe. Inawezekana unaishi maisha kama ya kitumwa lakini mkono wa Bwana uko pamoja na wewe. Yusufu alikuwa na Mungu kwenye kila mazingira toka anauzwa, alipopelekwa mahakamani kwa sababu ya mke wa Potifa Mungu alikuwa pamija nae. Alipokuwa jela alikuwa pamoja na Mungu kwa hiyo kila sehemu Mungu alikuwa pamoja nae. Kwa hiyo usije ukafikiri waliofungwa jela hawana Mungu wako pamoja na Bwana. Shetani alikuwa anagombana na akili za Yusufu ili zisipate nafasi ya kutumika maana alikuwa ana akili ya kusaidia familia yake lakini alinyimwa heshima nyumbani kwake. Akili alilozokuwa nazo Yusufu zilikuwa na uwezo wa kumsaidia baba yake lakini aliondolewa nyumbani kwao na kukatiwa mawasailiano na baba yake ili ajue kwamba amekufa. Shetani alikuwa akiwinda baba yake yaani mzee Yakobo asipate msaada wa akili za Yusufu. Unaweza ukawa unafurahia biashara uliyonayo na kufikiri kwamba umefika lakini Mungu ana kitu kikubwa kuliko unachofikiri. Ila hujajua kwamba huko ndani yako kuna kitu gani kimekaa na kwanini ndani yako unaona ndoto kubwa au unaona hujaridhika mahali ulipo kumbe Mungu anajaribu kukusukuma kukuonyesha kwamba ndani yako amekuwekea kitu kikubwa kuliko unacho fikiri. Hivyo usitosheke na mahali ulipo kisukume na usonge mbele na ukimwendea Mungu atakuonesha mahali unapotakiwa kuwa. Mungu alimpa Yusufu miaka 14 ya kutumia zile akili. Na ndiyo maana si suala la kuishi maisha marefu ni suala la kuishi katika mapenzi ya Mungu.
7/12/201910 minutes, 12 seconds
Episode Artwork

Akili za mwanadamu zingekuwaje kama tusingepitia dhambi, ungekuwa wapi sasa?

Jana tuliangalia kikwazo cha kwanza ni AKILI KUFUNGWA NA SHETANI na tukaangalia kwenye kile kitabu cha Luka 8:26 - 39 tukaangalia kwa undani pamoja na mistari mingine na maelezo kwa undani. Saa nyingine huwa nawaza sana namna akili ya mwanadamu ilivyo na ambavyo inafanya mambo makubwa je kama tusingepita kwenye dhambi ingekuwaje? Kwa sababu vitu vingi vimebuniwa na akili ya mwanadamu ambayo iko kwenye dhambi na ina kiwango cha kufanya kitu ilichokifanya, sasa fikiria kama asingekuwa na dhambi ingefanya vikubwa kiasi gani? Sijasoma kwenye Biblia, lakini najaribu kufikiria kuwa kama tukifika mbinguni halafu Mungu atatuonyesha tumetumia kiwango gani cha akili zetu alizotupa na tukajikuta tumetumia kiasi kidogo sana mfano ¼, au 5% au 10% na asilimia iliyobaki akatuonyesha kulikuwa na kitu gani .Pia hiyo akili ambayo haijatumika je tungeitumia tungekuwa na maisha ya aina gani. Nakuambia watu wengi wangekata rufaa ya kurudi duniani kwa sababu ndani yake wangegundua kuwa kuna vitu vikubwa sana. Tukiangalia mfano wa Yusufu mtoto wa mzee Yakobo kwenye Mwanzo 41, aliitwa ofisini kwa Farao kutafsiri ndoto ya Farao aliyoiota usiku na kurudia mara mbili. Mara ya kwanza Farao aliota ng'ombe wanono saba halafu wakaja wengine waliokonda kutoka kwenye mto. Wale waliokonda wakawala wale wenye afya na hata baada ya kuwala wakabaki wamekonda vile vile, akaamka; akalala na kuota ndoto nyingine akaona masuke na asubuhi yake akatafuta msaada wa tafsiri kila kona kwa waganga, wachawi na wenye hekima ili wamsaidie. Mpaka mfanyakazi wake akaeleza alivyokutana na Yusufu jela na namna alivyo weza kuwatafsiria ndoto zao. Baada ya kusikia habari ya Yusufu ndipo Farao akaagizwa Yusufu aitwe mbele zake.Yusufu alipopewa taarifa za kuitwa kwa Farao tunona akamtafsiria Farao ndoto zake na kumweleza juu ya ujio wa miaka 7 ya chakula na unono. Baada ya pale Farao akata kujua zaidi miaka 7 ya njaa. Aliambiwa hiyo njaa itakuwa kubwa mno kiasi ambacho miaka 7 ya unono itaonekana kama haikuwepo ndio maana aliona ng'ombe waliokonda wakiwala walionona. Baada ya kuwala wale ng’ombe , wale waliokonda hawakunenepa ili kuonyesha kuwa kipindi cha njaa kitakuwa kibaya sana. Yusufu alipomaliza kumtafsiria Farao ndoto alimwelezea kitu cha kufanya kwa sababu alikuwa anajiandaa kurudi jela. Alimwambia Farao “tafuta mtu mwenye akili na hekima umweke kwenye nafasi afanye yafuatayo
7/11/20199 minutes, 55 seconds
Episode Artwork

Tumia sala hii kuachilia Damu ya Yesu ifungue akili yako

Weka mikono yako juu ya kichwa ili tufanye maombi ambayo Mungu atafuatilia muunganiko wa ubongo wako na akili zako. Kama kuna mapepo katika akili zako yataachia tu kwa jina la Yesu. Omba Mungu aponye akili zako na kuweka huo muunganiko vizuri kwa Damu ya Yesu. Nyunyiza Damu ya Yesu juu yako. Pia kama hujaokoka hakikisha unaokoka, angalia link ya sala ya Toba na kitabu cha Hongera kwa kuokoka. Pia kama una ndugu yako unataka Mungu amponye akili zake andika jina lake tuma kwa namba za maombi tulizokuweka pale juu mwanzo wa somo hili. Kwa taarifa zaidi na kutoa sadaka kwa Mwalimu Christopher Mwakasege NAMBA ZA SADAKA NA MAOMBI 👉🏼 https://goo.gl/7XcFiP NAMNA YA KUPATA KANDA, CDs & DVDs BONYEZA HAPA 👉🏼 https://goo.gl/xrSwmN MAOMBI YA KUOKOKA NA KITABU CHA HONGERA KWA KUOKOKA. 👉🏼 https://goo.gl/XKoJNB
7/10/201910 minutes, 58 seconds
Episode Artwork

Uko mahali kwenye maisha yako kila kitu kimesimama, Yesu anakutafuta

Hii unaweza ukasikia mtu akisema “nimemlea huyu mtoto nikifikiri akili anazo kumbe hana”. Ukishasikia lugha ya nmna hiyo ina maana akili hazifanyi kazi inayotakiwa kwa sababu hamna mtu ambaye hana akili ila kuna namna zimebanwa. Sasa angalia yule kijana wa nchi ya Wagerasi kila mtu alikuwa kamkatia tamaa. Sasa Yesu alikuwa hafanyi jambo lolote isipokuwa kamuomba baba akifanya. Kwa hiyo walikuwa anafanya mapenzi yake maana alikuwa akimuona Yesu kayakamilisha. Yesu aliposema tuvuke mpaka ng’ambo ina maana aliuacha mkutano mkubwa alafu akaingia katika boti kwenda ng’ambo mpaka nchi ya Wagerasi. Wanafunzi wake walikuwa hawajui wanaenda kufanya nini huko lakini Roho Mtakatifu alikuwa anajua kwamba kuna mtu yupo makaburini hapati hata msaada maana tunaona hakupelekwa na watu kwa Yesu. Maandiko yanatuambia kuwa Yesu alipofika tu alianza kukemea mapepo na ndio maana yalianza kupiga kelele kuwa tuna nini na wewe Yesu. Yesu alimfuatilia yule kijana maana tunaona hamna mtu aliyempeleka kwa Yesu kwa sababu kulikuwa na mkutano ng’ambo ya ziwa kwa sababu wangekuwa na haja ya kumpeleka wangempeleka kwa Yesu alipokuwa ng’ambo maana boti zilikuwepo za kuweza kuwavusha hata ng’ambo ya pili. Kila mtu alikuwa amemuacha na hapati msaada hata ndugu zake hawakumsaidia. Unisikilize inawezekana kabisa uko mahali na kila kitu chako kimekwama, nipo hapa kukuambia neno la Bwana kuwa Yesu yupo ng’ambo na atakuja kukufuata na wewe ili aje kukutembelea. Haijalishi maisha yako yako mahali pagumu kiasi gani kama vile makaburini Yesu atakuja yeye mwenyewe kukufuata hata kama haujakaribishwa kwenye mkutano. Yesu alipomfuata yule kijana alihusika moja kwa moja na akili zake maana alijua kabisa ya kwamba yule kijana akifunguliwa akili tu anaweza akasimama peke yake. Yule kijana alipoponywa biblia inatuambia alivaa nguo. Sasa swali linakuja hizo nguo alizipata wapi? Kwa hiyo inawezekana kabisa hakuchana nguo zote bali alikuwa anavua kila akivalishwa. Maana hatuoni kama kuna mtu alimpa nguo hata watu wa pale maana hata Yesu mwenyewe hakuja na nguo wala wanafunzi wake za kumpa yule kijana. Biblia inatuambia kuwa wanakijiji walipokuja walimkuta tayari kavaa nguo. Wafugaji wa pale walioopona nguruwe wamejimwaga baharini walikimbia mtaani kuwaeleza watu. Sasa yule kijana akili zake ziliporudi alitafuta nguo zake. Sasa akili zikifanya kazi jamii itakupa heshima hata kama haitaki. Biblia inatuambia kuwa walipokuja walimkuta yule kijana aliyekuwa na pepo kavaa nguo zake na katulia pale na akili zake zikiwa vizuri waliogopa sana. Baada ya hapo walimuomba Yesu aondoke kwao, na Yesu alitii aliondoka akapanda boti na akarudi kwenye mkutano. Mungu anaweza akaleta semina hii kwa ajili yako tu. Kwa hiyo isikusumbue umati wa watu bali angalia kama Yesu amekutembelea au hajakutembelea. Kuna watu kwenye biblia tunaona watu waliokuwa wanaleta wagonjwa kwa Yesu ili wapate msaada lakini yule kijana wa nchi ya Wagerasi hakuna aliyempeleka kwa Yesu. Labda inawezekana watu walimuogopa kwa sababu alikuwa mgomvi na ana mapepo. Sasa inawezekana kuna mtu wa namna hiyo nyumbani kwenu ambaye mnasema mtu huyu anakua mwili tu ila akili hamna na mnamkalia na kikao kabisa kwa ajili yake maana mna wasi wasi na akili zake. Kuna watu wengi sana ambao shetani kabana akili zao na za ndugu zao maana shetani hafungi mwili tu bali anafunga na akili pia. Shetani anaweza akalenga kufunga akili zenyewe kwa sababu ya umuhimu wake kwa sababu atakuwa ameshika sehemu kubwa sana ya akili yake na anakwamisha maisha yake. Kuna mtu unakuta kasoma vizuri sana na ana degree mbili hivi au tatu. Anaanza kazi vizuri kabisa lakini baada ya muda anaacha. Ukimwuliza kwanini atakuambia kuwa huku kazini wananisumbua sumbua tu. Sasa unamwuliza sasa utafanya nini sasa anasema nitafanya biashara. Hapo mtaji hana, hana hata uzoefu wa biashara, kakaa tu hapo nyumbani ila anasema nitafanya biashara. Baada ya hapo utamuona anaanza kuingia kwenye vijiwe na kukaa na watu huko. Hii ni kwa sababu akili zinafanana na anao kaa nao maana akili huwa zinaitana. Biblia inasema aonavyo nafsini mwake ndivyo alivyo. Kwa hiyo kama unataka kubadili maisha yako tazama wanaokuzunguka. Kwa sababu kama wanafanana na wewe katika kufikiri. Kama unawapenda sana kaa nao mbali kwanza alafu alafu ukikaa sawa ndipo uje uwatoe kama gari iliyokwama kwenye matope. Maana hamuwezi kusaidiana wote mkiwa kwenye matope, Ondoka kwanza kwenye kijiwe katafute msaada kwa Yesu, na ukirudi ukiwa umebadikika ndipo uje uwatoe kwenye kijiwe. Kwa sababu wataona namna kufikiri kwako na kuwaza kwako kulivyobadilika kwa sababu kuna kitu Mungu amefanya kwenye akili zako na zimefunguliwa.
7/9/20199 minutes, 59 seconds
Episode Artwork

Unapookoka neno la mungu huanza kushughulikia akili zako

1 Petro 2:1-2 “Basi, wekeni mbali uovu wote na hila yote, na unafiki na husuda na masingizio yote. Kama watoto wachanga waliozaliwa sasa yatamanini maziwa ya akili yasiyoghoshiwa, ili kwa hayo mpate kuukulia wokovu;” Hakusema maziwa ya Roho amesema maziwa ya akili, Neno la Mungu unalopewa unapookoka mahali pa kushughulika napo pa kwanza ni akili zako ili upate kuukulia wokovu, ndio maana akili zikibanwa haijalishi umeokoka miaka mingapi huwezi kukua kiroho, ndio maana huwezi kujivunia miaka uliyokaa ndani ya wokovu, Mungu anaangalia umekua kiasi gani na usipojua kwamba Mungu kaziweka akili kwa makusudi kabisa macho na ubongo vitakusaidia kusoma Biblia lakini haviwezi vikakusaidia kuelewa. Mathayo 7:24 “Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba;mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba. Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga; mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa.” Huyu ni Yesu anazungumza anasema mtendaji wa Neno amefaninishwa na mtu mwenye akili hajasema amefananishwa na wa kiroho. Watu wengi sana hawajui namna ya kuunganisha akili na imani, wanafikiri mtu aliyeokoka akitumia akili anaenda kimwili na sasa umeelewa kwamba akili haziko kwenye mwili, Biblia imekataza tusizitegemee akili lakini tuzitumie akili. Yule mtu ambaye alikuwa na kichaa alipofunguliwa yale mapepo wale watu kwenye kijiji walikuja kumtazama pamoja nakumwona amevaa nguo na ana utulivu wakagundua ana akili zake. Maana yake walitambua ya kwamba huyu mtu maisha aliyokuwa anaishi akili hazikuwa kazini. Ukisoma hiyo mistari vizuri kwa jicho la mwalimu kuna kitu hapo utaona Luka 8:22,37 “Ikawa siku zile mojawapo alipanda chomboni yeye na wanafunzi wake, akawaambia, Na tuvuke mpaka ng’ambo ya ziwa. Wakatweka matanga. Na jamii ya watu wa nchi ya Wagerasi iliyo kando kando walimwomba aondoke kwao, kwa kuwa walishikwa na hofu nyingi; basi akapanda chomboni, akarudi.” Roho Mtakatifu alimbana Yesu wakati huduma ilikuwa inaendelea ukitazama pale aliporudi mkutano ulimkaribisha kwa furaha kwa maana walimgojea wote utafikiri aliwaambia kuna jambo naenda kuangalia narudi sasa hivi, maana aliporudi tena ng’ambo mkutano mkubwa ulikuwa unamgojea. Yule mtu Biblia haituambii jina lake lakini mbingu zilikuwa zinamfahamu na maandiko yanatuambia alikuwa na kwao kwa sababu alipotaka kumfuata akamwambia nenda rudi nyumbani kwako. Inawezekana alikuwa na wazazi, alikuwa na ndugu alikuwa na majirani, alikuwa pia na marafiki lakini mazingira yalimbana kiasi kwamba akawa anashinda makaburini na milimani na maandiko yanasema kuna kipindi ilibidi afungwe ili kuweza kuhimili ile vurugu ambayo alikuwa anafanya. Inawezekana wote walimkatia tamaa na yale mapepo yalikuwa ndani ya mtu na yalikuwa yanamkwamisha yeye mwenyewe maana anakimbilia kufanya vitu na yanamkwamisha. Maana tunaona mapepo baada ya kutoka yaliingia ndani ya nguruwe na kuwapeleka majini kwa kasi. Sasa haya mapepo ndio yalikuwa ndani ya mtu yakimsukumia wazo la kufanya na kinamharibu na kumwamisha jumla kabisa. Hii unaweza ukasikia mtu akisema “nimemlea huyu mtoto nikifikiri akili anazo kumbe hana”. Ukishasikia lugha ya nmna hiyo ina maana akili hazifanyi kazi inayotakiwa kwa sababu hamna mtu ambaye hana akili ila kuna namna zimebanwa.
7/8/20199 minutes, 59 seconds
Episode Artwork

Nafsi na mwili viliumbwa vimilikiwe na roho

NAFSI NA MWILI VILIUMBWA VIMILIKIWE NA ROHO Zaburi 63:1 “Ee MUNGU, Mungu wangu, nitakutafuta mapema, Nafsi yangu inakuonea kiu, Mwili wangu wakuonea shauku, Katika nchi kame na uchovu, isiyo na maji.” Mwandishi anamwambia Mungu, “Mungu wangu nitakutafuta mapema”, anaposema nitakutafuta ni roho ya Daudi inamweleza Mungu ya kwamba nitakutafuta mapema. Roho hiyo hiyo inasema kwa niaba ya nafsi, inasema nafsi yangu inakuonea kiu, lakini pia inasema kwa niaba ya mwili inasema mwili wangu wakuonea shauku. Nilitaka uone ya kwamba hauwezi kusema nafsi yangu kama haijapangiwa imilikiwe na roho na hauwezi kusema mwili wangu kama roho haikupangiwa kumiliki mwili. Ni dhambi iliyokuja na kukorofisha utaratibu wa uumbaji na mwili ukaonekana kama ndio unao tawala kila kitu, lakini Mungu aliweka kwa makusudi kabisa kwamba roho ya mtu ndiyo imiliki nafsi na mwili. AKILI IMO NDANI YA NAFSI Ayubu 32:8 “Lakini imo roho ndani ya mwanadamu, Na pumzi za Mwenyezi huwapa akili.” Unganisha na kile kitabu cha Mwanzo ili uelewe vizuri zaidi: Mwanzo 2:7 “Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.” Kwa hiyo kama pumzi iliachilia nafsi ndani ya mtu na pumzi iliachilia akili ndani ya mtu kwa hiyo akili imo ndani ya nafsi. Akili tumeipata kwa msaada wa pumzi ya Mungu na nafsi tumeipata kwa msaada wa pumzi ya Mungu. Wakati nafsi inaingizwa ndani yetu na akili ziliingizwa, na ndiyo maana kama unayo nafsi lazima na akili unazo, hakuna mtu ambaye ameumbwa bila akili, ile kwamba huzitumii haina maana kwamba huna. AKILI SIO UBONGO, LAKINI MUNGU ALIVIUMBA VIFANYE KAZI KWA KUSHIRIKIANA Biblia ya Kiswahili inafundisha vizuri zaidi juu ya akili kuliko Biblia ya Kiingereza. Ukisoma Biblia ya Kiingereza unahitaji kuwa mwangalifu sana kutafuta neno akili kwa sababu limeandikwa kwa tafsiri tofauti tofauti kutegemeana na waliokuwa wakitafsiri na inategemea pia picha nzima ya habari inayozungumzwa. Kwa sababu ubongo kwenye Kiingereza wanasema ni Brain lakini wengine wanasema ni Brains wengine wanasema ni intelligence na wengine wanasema ni mind lakini kwenye Biblia ya Kiswahili wamenyooka na kupata neno nzuri kabisa ambalo ni akili. Ubongo upo kwenye mwili na akili ipo kwenye nafsi. Na ndiyo maana hata ukienda hospitali wataalam watakuambia ubongo ulipo lakini watapata shida sana kukueleza akili zilipo. Mungu aliumba akili na ubongo vifanye kazi pamoja lakini akili imo ndani ya nafsi na ubongo umo ndani ya mwili. Kazi ya ubongo ni kupokea elimu na kazi ya akili ni kuchukua elimu na kuibadilisha kuwa maarifa Ubongo haubadilishagi elimu kuwa maarifa. Na ndiyo maana ukishikwa akili zako hata kama una akili kiasi gani ubongo unaweza kukusaidia ukafaulu darasani lakini huwezi kufaulu kwenye maisha. Kwa sababu maisha hayafaulishwi na ubongo wako bali ufaulishwa na akili yako na nafsi yako. Biblia inasema watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa na sio kwa kukosa ubongo. Na ndiyo maana mtu anaweza kuwa na shahada kadhaa lakini maisha hana. Ile tu kwamba mtu amesoma haina maana kisomo kinampa maisha. Kisomo kinaweza kikakupa cheti, kazi, heshima kwenye jamii lakini hakiwezi kikakupa maisha kwa sababu maisha yalinyang’anywa dhambi ilipoingia maana mwanadamu hakupewa maisha ya kwake alipewa maisha ya Mungu ambayo yanaitwa uzima. Yesu alisema nimekuja ili wawe na uzima kisha wawe nao tele. Huwezi kupata maisha ambayo Mungu aliyakusudia nje ya Yesu. Ubongo unapokea habari/information lakini akili inageuza habari kuwa ufahamu Haisemi ndipo akawafunulia akili zao wapate kusoma maandiko, kusoma hakuna shida, unaweza kusoma Biblia, ukakariri na kuimaliza yote lakini kuielewa akili lazima iingie kazini.
7/7/20199 minutes, 59 seconds
Episode Artwork

Akili kufungwa na shetani ili usifikie malengo yako

AKILI KUFUNGWA NA SHETANI. Luka 8:26‭-‬39 “Wakafika pwani ya nchi ya Wagerasi, inayoelekea Galilaya. Naye aliposhuka pwani, alikutana na mtu mmoja wa mji ule, mwenye pepo, hakuvaa nguo siku nyingi, wala hakukaa nyumbani, ila makaburini. Alipomwona Yesu alipiga kelele, akaanguka mbele yake, akasema kwa sauti kuu, Nina nini nawe, Yesu, Mwana wa Mungu aliye juu? Nakusihi usinitese. Kwa kuwa amemwamuru yule pepo mchafu amtoke mtu yule. Maana amepagawa naye mara nyingi, hata alilindwa kifungoni na kufungwa minyororo na pingu; akavikata vile vifungo, akakimbizwa jangwani kwa nguvu za yule pepo. Yesu akamwuliza, Jina lako nani? Akasema, Jina langu ni Jeshi; kwa sababu pepo wengi wamemwingia. Wakamsihi asiwaamuru watoke kwenda shimoni. Basi, hapo palikuwa na kundi la nguruwe wengi wakilisha mlimani; wakamsihi awape ruhusa kuwaingia wale. Akawapa ruhusa. Pepo wakamtoka mtu yule wakawaingia nguruwe, nalo kundi lilitelemka gengeni kwa kasi, wakaingia ziwani, wakafa maji. Wachungaji walipoona lililotokea walikimbia, wakaieneza habari mjini na mashambani. Watu wakatoka kwenda kuliona lililotokea, wakamwendea Yesu, wakamwona mtu yule aliyetokwa na pepo ameketi miguuni pa Yesu, amevaa nguo, ana akili zake; wakaogopa. Na wale waliokuwa wameona waliwaeleza jinsi alivyoponywa yule aliyepagawa na pepo. Na jamii ya watu wa nchi ya Wagerasi iliyo kando kando walimwomba aondoke kwao, kwa kuwa walishikwa na hofu nyingi; basi akapanda chomboni, akarudi. Na mtu yule aliyetokwa na pepo alimwomba ruhusa afuatane naye; lakini yeye alimwaga akisema, Rudi nyumbani kwako, ukahubiri yalivyo makuu Mungu aliyokutendea. Akaenda zake, akihubiri katika mji wote, yalivyo makuu mambo aliyotendewa na Yesu.” Tunataka kuangalia hiki kikwazo cha akili kufungwa katika malengo ya maisha ya mtu. Tunamwona huyu mtu akili zake zilifungwa ingawa mapepo yalikuwa mengi sana juu yake lakini mapepo hayo yalilenga kushika na kufunga akili zake ili zisifanye kazi inayotakiwa na aliishi kama mtu asiye na akili kabisa . Ili tuliangalie hiki kikwazo kuna mambo kadhaa tunapaswa tufahamu kwa undani kuhusu akili ili upate kuelewa kama umekwama hapo Mungu aweze kukufungua. JAMBO LA KWANZA. MTU NI ROHO, ANAYO NAFSI ANAKAA NDANI YA MWILI. 2 Wakorintho 7:1 “Basi, wapenzi wangu, kwa kuwa tuna ahadi hizo, na tujitakase nafsi zetu na uchafu wote wa mwili na roho, huku tukitimiza utakatifu katika kumcha Mungu.” Nataka tuone vitu vitatu hapo yaani NAFSI, ROHO NA MWILI. Ukisoma pia Zaburi 42:5 “Nafsi yangu, kwa nini kuinama, Na kufadhaika ndani yangu? Umtumaini Mungu; Kwa maana nitakuja kumsifu, Aliye afya ya uso wangu, Na Mungu wangu.” Hapo anayesema “Nafsi yangu…” ni roho ya Daudi kwamba inataka kutuambia inayo nafsi na hiyo nafsi inakaa ndani yake. Kwa hiyo mtu ki roho anayo nafsi na anakaa ndani ya mwili. JAMBO LA PILI 2. ROHO YA MTU ILIUMBWA KWANZA HALAFU UKAUMBWA MWILI NDIPO NAFSI IKAUMBWA. Mwanzo 2:7 “BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.” Mwanzo 1:27 “Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba.” Sura ya pili inatuambia hakukuwa na mtu wa kuilima ardhi kwa hiyo Mungu hakuinyeshea mvua ardhi. Sura ya kwanza inasema Mungu alimuumba mtu kwa mfano wake mwanamume na mwanamke aliwaumba. Lazima uzisome hizi sura mbili kwa pamoja kila sura kwa wakati mmoja maana ukisoma moja moja zitakusumbua kwenye uumbaji. Maana ukitaka kufahamu jinsi uumbaji ulivyoenda sawa ni lazima usome hizi sura zote mbili kwa pamoja maana zinaenda pamoja Sura ya kwanza Mungu alimuumba mtu roho, yaani roho yake ndipo ilipoumbwa, aliumba kwa mfano wake mwanamume na mwanamke wote roho zao ziliumbwa sura ya kwanza. Sura ya pili unaona vitu vyote vilivyokuwa vikitamkwa kwenye sura ya kwanza huvioni. Hakukuwa na mche wowote kondeni wakati kule mwanzo kulikuwa na miti na kila kitu vizae na alizungumza juu ya wanyama, ndege na n.k lakini kwenye sura ya pili huvioni unaona vyote vinatoka kwenye udongo. Alikuwa anatengeneza miili yao. Maana mtu alipoumbwa mwanzoni walipewa mwili mmoja mwanamume na mwanamke waliishi kwenye mwili mmoja.
7/6/20199 minutes, 59 seconds